< Zaburi 81 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
For the Chief Musician. On an instrument of Gath. By Asaph. Sing aloud to God, our strength! Make a joyful shout to the God of Jacob!
2 Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
Raise a song, and bring here the tambourine, the pleasant lyre with the harp.
3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
Blow the trumpet at the New Moon, at the full moon, on our feast day.
4 hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
For it is a statute for Israel, an ordinance of the God of Jacob.
5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
He appointed it in Joseph for a covenant, when he went out over the land of Egypt, I heard a language that I did not know.
6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
“I removed his shoulder from the burden. His hands were freed from the basket.
7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
You called in trouble, and I delivered you. I answered you in the secret place of thunder. I tested you at the waters of Meribah.” (Selah)
8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
“Hear, my people, and I will testify to you, Israel, if you would listen to me!
9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
There shall be no strange god in you, neither shall you worship any foreign god.
10 Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
I am the LORD, your God, who brought you up out of the land of Egypt. Open your mouth wide, and I will fill it.
11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
But my people did not listen to my voice. Israel desired none of me.
12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
So I let them go after the stubbornness of their hearts, that they might walk in their own counsels.
13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
Oh that my people would listen to me, that Israel would walk in my ways!
14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
I would soon subdue their enemies, and turn my hand against their adversaries.
15 Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
The haters of the LORD would cringe before him, and their punishment would last forever.
16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
But he would have also fed them with the finest of the wheat. I will satisfy you with honey out of the rock.”

< Zaburi 81 >