< Zaburi 80 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
Escucha, oh Guardián de Israel, guiando a José como un rebaño; tú que tienes tu asiento con los ángeles. deja que se vea tu gloria.
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
Delante de Efraín, de Benjamín y de Manasés, despierta de tu sueño, y ven a salvarnos.
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Llévanos de nuevo, oh Dios; veamos el brillo de tu rostro y déjanos estar a salvo.
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
Oh Jehová Dios de los ejércitos, ¿hasta cuándo se encenderá tu ira contra la oración de tu pueblo?
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
Les diste el pan de llanto para comer; por su bebida les has dado tristeza en gran medida.
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
Nos haces causa de guerra entre nuestros vecinos; nuestros enemigos se están riendo de nosotros entre ellos.
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
Llévanos de nuevo, oh Dios de los ejércitos; veamos el brillo de tu rostro y déjanos estar a salvo.
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
Sacaste una vid de Egipto, expulsando a las naciones y plantando en su tierra.
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
Preparó un lugar para ello, para que arraigara profundamente, y envió sus ramas sobre toda la tierra.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
Las montañas estaban cubiertas con su sombra, y los grandes árboles con sus ramas.
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
Envió sus armas al mar, y sus ramas al río.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
¿Por qué derribar sus muros con tus manos, para que todos los que pasan puedan tomar su fruto?
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
Es desarraigado por los cerdos del bosque, las bestias del campo obtienen su alimento de él.
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
Vuelve, oh Dios de los ejércitos: desde el cielo vuelven tus ojos a esta vid, y concéntrate en ella,
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Hasta el árbol que fue plantado a tu diestra, y al árbol que para ti afirmaste.
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
Se quema con fuego; es cortado: son destruidos por la ira de tu rostro.
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Sea tu mano sobre el varón de tu diestra, sobre el hijo de hombre, que para ti afirmaste.
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
Así no nos apartaremos de ti; guárdanos en la vida y alabaremos tu nombre.
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Llévanos, oh Jehová Dios de los ejércitos; restáuranos! veamos el brillo de tu rostro y déjanos estar a salvo.