< Zaburi 80 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
Al Músico principal: sobre Sosannim Eduth: Salmo de Asaph. OH Pastor de Israel, escucha: tú que pastoreas como á ovejas á José, que estás entre querubines, resplandece.
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
Despierta tu valentía delante de Ephraim, y de Benjamín, y de Manasés, y ven á salvarnos.
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Oh Dios, haznos tornar; y haz resplandecer tu rostro, y seremos salvos.
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
Jehová, Dios de los ejércitos, ¿hasta cuándo humearás tú contra la oración de tu pueblo?
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
Dísteles á comer pan de lágrimas, y dísteles á beber lágrimas en gran abundancia.
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
Pusístenos por contienda á nuestros vecinos: y nuestros enemigos se burlan entre sí.
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
Oh Dios de los ejércitos, haznos tornar; y haz resplandecer tu rostro, y seremos salvos.
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
Hiciste venir una vid de Egipto: echaste las gentes, y plantástela.
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
Limpiaste [sitio] delante de ella, é hiciste arraigar sus raíces, y llenó la tierra.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
Los montes fueron cubiertos de su sombra; y sus sarmientos [como] cedros de Dios.
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
Extendió sus vástagos hasta la mar, y hasta el río sus mugrones.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
¿Por qué aportillaste sus vallados, y la vendimian todos los que pasan por el camino?
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
Estropeóla el puerco montés, y pacióla la bestia del campo.
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
Oh Dios de los ejércitos, vuelve ahora: mira desde el cielo, y considera, y visita esta viña,
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Y la planta que plantó tu diestra, y el renuevo que para ti corroboraste.
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
Quemada á fuego está, asolada: perezcan por la reprensión de tu rostro.
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Sea tu mano sobre el varón de tu diestra, sobre el hijo del hombre que para ti corroboraste.
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
Así no nos volveremos de ti: vida nos darás, é invocaremos tu nombre.
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Oh Jehová, Dios de los ejércitos, haznos tornar; haz resplandecer tu rostro, y seremos salvos.

< Zaburi 80 >