< Zaburi 80 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
In finem, Pro iis, qui commutabuntur, testimonium Asaph, Psalmus. Qui regis Israel, intende: qui deducis velut ovem Ioseph. Qui sedes super cherubim, manifestare
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
coram Ephraim, Beniamin, et Manasse. Excita potentiam tuam, et veni, ut salvos facias nos.
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Deus converte nos: et ostende faciem tuam, et salvi erimus.
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
Domine Deus virtutum, quousque irasceris super orationem servi tui?
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
Cibabis nos pane lacrymarum: et potum dabis nobis in lacrymis in mensura?
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
Posuisti nos in contradictionem vicinis nostris: et inimici nostri subsannaverunt nos.
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
Deus virtutum converte nos: et ostende faciem tuam: et salvi erimus.
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
Vineam de Ægypto transtulisti: eiecisti Gentes, et plantasti eam.
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
Dux itineris fuisti in conspectu eius: plantasti radices eius, et implevit terram.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
Operuit montes umbra eius: et arbusta eius cedros Dei.
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
Extendit palmites suos usque ad mare: et usque ad flumen propagines eius.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
Ut quid destruxisti maceriam eius: et vindemiant eam omnes, qui prætergrediuntur viam?
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
Exterminavit eam aper de silva: et singularis ferus depastus est eam.
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
Deus virtutum convertere: respice de cælo, et vide, et visita vineam istam.
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Et perfice eam, quam plantavit dextera tua: et super filium hominis, quem confirmasti tibi.
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
Incensa igni, et suffossa ab increpatione vultus tui peribunt.
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Fiat manus tua super virum dexteræ tuæ: et super filium hominis, quem confirmasti tibi.
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
Et non discedimus a te, vivificabis nos: et nomen tuum invocabimus.
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Domine Deus virtutum converte nos: et ostende faciem tuam, et salvi erimus.

< Zaburi 80 >