< Zaburi 80 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
Al maestro del coro. Su «Giglio del precetto». Di Asaf. Salmo. Tu, pastore d'Israele, ascolta, tu che guidi Giuseppe come un gregge. Assiso sui cherubini rifulgi
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
davanti a Efraim, Beniamino e Manasse. Risveglia la tua potenza e vieni in nostro soccorso.
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Rialzaci, Signore, nostro Dio, fà splendere il tuo volto e noi saremo salvi.
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
Signore, Dio degli eserciti, fino a quando fremerai di sdegno contro le preghiere del tuo popolo?
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
Tu ci nutri con pane di lacrime, ci fai bere lacrime in abbondanza.
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
Ci hai fatto motivo di contesa per i vicini, e i nostri nemici ridono di noi.
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
Rialzaci, Dio degli eserciti, fà risplendere il tuo volto e noi saremo salvi.
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
Hai divelto una vite dall'Egitto, per trapiantarla hai espulso i popoli.
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
Le hai preparato il terreno, hai affondato le sue radici e ha riempito la terra.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
La sua ombra copriva le montagne e i suoi rami i più alti cedri.
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
Ha esteso i suoi tralci fino al mare e arrivavano al fiume i suoi germogli.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
Perché hai abbattuto la sua cinta e ogni viandante ne fa vendemmia?
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
La devasta il cinghiale del bosco e se ne pasce l'animale selvatico.
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
Dio degli eserciti, volgiti, guarda dal cielo e vedi e visita questa vigna,
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
proteggi il ceppo che la tua destra ha piantato, il germoglio che ti sei coltivato.
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
Quelli che l'arsero col fuoco e la recisero, periranno alla minaccia del tuo volto.
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Sia la tua mano sull'uomo della tua destra, sul figlio dell'uomo che per te hai reso forte.
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
Da te più non ci allontaneremo, ci farai vivere e invocheremo il tuo nome.
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Rialzaci, Signore, Dio degli eserciti, fà splendere il tuo volto e noi saremo salvi.