< Zaburi 80 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
Dem Musikmeister, nach “Lilien”. Ein Zeugnis Asaphs. Ein Psalm. Hirte Israels, vernimm! Der du Joseph leitest, wie Schafe, der du über den Keruben thronst, glänze auf!
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
Vor Ephraim und Benjamin und Manasse her biete deine Macht auf und komm uns zu Hilfe!
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Gott, stelle uns wieder her und laß dein Angesicht leuchten, daß uns geholfen werde!
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
Jahwe, Gott der Heerscharen, wie lange zürnst du bei dem Gebete deines Volks?
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
Du speistest sie mit Thränenbrot und tränktest sie in reichem Maße mit Thränen.
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
Du machtest uns zum Zankapfel für unsere Nachbarn, und unsere Feinde treiben ihren Spott.
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
Gott der Heerscharen, stelle uns wieder her und laß dein Angesicht leuchten, daß uns geholfen werde!
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
Einen Weinstock hobst du aus Ägypten aus, vertriebst Heiden und pflanztest ihn dafür ein.
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
Du machtest Raum vor ihm, und er wurzelte ein und füllte das Land.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
Die Berge wurden von seinem Schatten bedeckt, und die Cedern Gottes von seinen Zweigen.
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
Er entsandte seine Ranken bis ans Meer und seine Schößlinge bis zum Euphratstrom.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
Warum hast du seine Mauern eingerissen, daß ihn alle, die des Wegs vorüberkommen, zerpflücken?
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
Der Eber aus dem Walde frißt ihn ab, und was sich auf dem Felde regt, weidet ihn ab.
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
Gott der Heerscharen, kehre doch wieder! Blicke vom Himmel herab und sieh darein und nimm dich dieses Weinstocks an
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
und des Setzlings, den deine Rechte gepflanzt, und des Schößlings, den du dir kräftig aufgezogen hast!
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
Er ist mit Feuer verbrannt, ist abgeschnitten; vor dem Drohen deines Angesichts vergehen sie!
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Deine Hand sei über dem Manne deiner Rechten, über dem Menschensohne, den du dir kräftig aufgezogen hast.
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
So wollen wir nicht von dir weichen! Erhalte uns am Leben, so wollen wir deinen Namen anrufen!
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Jahwe, Gott der Heerscharen, stelle uns wieder her! Laß dein Angesicht leuchten, daß uns geholfen werde!

< Zaburi 80 >