< Zaburi 80 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
Psaume d'Asaph, [donné] au maître chantre, [pour le chanter] sur Sosannim-héduth. Toi qui pais Israël, prête l'oreille, toi qui mènes Joseph comme un troupeau, toi qui es assis entre les Chérubins, fais reluire ta splendeur.
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
Réveille ta puissance au-devant d'Ephraïm, de Benjamin, et de Manassé; et viens pour notre délivrance.
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Ô Dieu! ramène-nous, et fais reluire ta face; et nous serons délivrés.
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
Ô Eternel, Dieu des armées, jusques à quand seras-tu irrité contre la requête de ton peuple?
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
Tu les as nourris de pain de larmes, et tu les as abreuvés de pleurs à grande mesure.
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
Tu nous as mis pour un sujet de dispute entre nos voisins, et nos ennemis se moquent de nous entre eux.
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
Ô Dieu des armées ramène-nous, et fais reluire ta face; et nous serons délivrés.
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
Tu avais transporté une vigne hors d'Egypte; tu avais chassé les nations, et tu l'avais plantée.
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
Tu avais préparé une place devant elle, tu lui avais fait prendre racine, et elle avait rempli la terre.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
Les montagnes étaient couvertes de son ombre, et ses rameaux étaient [comme] de hauts cèdres.
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
Elle avait étendu ses branches jusqu'à la mer, et ses rejetons jusqu'au fleuve.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
Pourquoi as-tu rompu ses cloisons, de sorte que tous les passants en ont cueilli les raisins?
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
Les sangliers de la forêt l'ont détruite, et toutes sortes de bêtes sauvages l'ont broutée.
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
Ô Dieu des armées retourne, je te prie; regarde des cieux, vois, et visite cette vigne;
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Et le plant que ta droite avait planté, et les provins que tu avais fait devenir forts pour toi.
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
Elle est brûlée par feu, elle est retranchée; ils périssent dès que tu te montres pour les tancer.
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Que ta main soit sur l'homme de ta droite, sur le fils de l'homme que tu t'es fortifié.
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
Et nous ne nous retirerons point arrière de toi. Rends-nous la vie, et nous invoquerons ton Nom.
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Ô Eternel! Dieu des armées, ramène-nous, [et] fais reluire ta face; et nous serons délivrés.