< Zaburi 80 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
Au chef des chantres. Sur les lis lyriques. D’Asaph. Psaume. Prête l’oreille, berger d’Israël, Toi qui conduis Joseph comme un troupeau! Parais dans ta splendeur, Toi qui es assis sur les chérubins!
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
Devant Éphraïm, Benjamin et Manassé, réveille ta force, Et viens à notre secours!
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
O Dieu, relève-nous! Fais briller ta face, et nous serons sauvés!
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
Éternel, Dieu des armées! Jusques à quand t’irriteras-tu contre la prière de ton peuple?
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
Tu les nourris d’un pain de larmes. Tu les abreuves de larmes à pleine mesure.
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
Tu fais de nous un objet de discorde pour nos voisins, Et nos ennemis se raillent de nous.
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
Dieu des armées, relève-nous! Fais briller ta face, et nous serons sauvés!
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
Tu avais arraché de l’Égypte une vigne; Tu as chassé des nations, et tu l’as plantée.
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
Tu as fait place devant elle: Elle a jeté des racines et rempli la terre;
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
Les montagnes étaient couvertes de son ombre, Et ses rameaux étaient comme des cèdres de Dieu;
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
Elle étendait ses branches jusqu’à la mer, Et ses rejetons jusqu’au fleuve.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
Pourquoi as-tu rompu ses clôtures, En sorte que tous les passants la dépouillent?
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
Le sanglier de la forêt la ronge, Et les bêtes des champs en font leur pâture.
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
Dieu des armées, reviens donc! Regarde du haut des cieux, et vois! Considère cette vigne!
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Protège ce que ta droite a planté, Et le fils que tu t’es choisi!…
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
Elle est brûlée par le feu, elle est coupée! Ils périssent devant ta face menaçante.
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Que ta main soit sur l’homme de ta droite, Sur le fils de l’homme que tu t’es choisi!
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
Et nous ne nous éloignerons plus de toi. Fais-nous revivre, et nous invoquerons ton nom.
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Éternel, Dieu des armées, relève-nous! Fais briller ta face, et nous serons sauvés!