< Zaburi 80 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
Au chef de musique. Sur Shoshannim. Témoignage d’Asaph. Psaume. Berger d’Israël! prête l’oreille. Toi qui mènes Joseph comme un troupeau, toi qui es assis entre les chérubins, fais luire ta splendeur!
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
Devant Éphraïm, et Benjamin, et Manassé, réveille ta puissance, et viens nous sauver!
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Ô Dieu! ramène-nous; et fais luire ta face, et nous serons sauvés.
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
Éternel, Dieu des armées! jusques à quand ta colère fumera-t-elle contre la prière de ton peuple?
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
Tu leur as fait manger un pain de larmes, et tu les as abreuvés de larmes à pleine mesure.
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
Tu as fait de nous un sujet de contestation pour nos voisins, et nos ennemis se moquent [de nous] entre eux.
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
Ô Dieu des armées! ramène-nous; et fais luire ta face, et nous serons sauvés.
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
Tu as transporté d’Égypte un cep; tu as chassé les nations, et tu l’as planté;
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
Tu as préparé une place devant lui, il a poussé des racines, et a rempli le pays.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
Les montagnes étaient couvertes de son ombre, et ses sarments étaient [comme] des cèdres de Dieu;
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
Il étendait ses pampres jusqu’à la mer, et ses pousses jusqu’au fleuve.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
Pourquoi as-tu rompu ses clôtures, de sorte que tous ceux qui passent le pillent?
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
Le sanglier de la forêt le déchire, et les bêtes des champs le broutent.
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
Ô Dieu des armées! retourne, je te prie; regarde des cieux, et vois, et visite ce cep,
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Et la plante que ta droite a plantée, et le provin que tu avais fortifié pour toi.
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
Elle est brûlée par le feu, elle est coupée; ils périssent, parce que tu les tances.
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Que ta main soit sur l’homme de ta droite, sur le fils de l’homme que tu as fortifié pour toi:
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
Et nous ne nous retirerons pas de toi. Fais-nous revivre, et nous invoquerons ton nom.
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Éternel, Dieu des armées! ramène-nous; fais luire ta face, et nous serons sauvés.

< Zaburi 80 >