< Zaburi 80 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
To victorie; this salm is witnessing of Asaph for lilies. Thou that gouernest Israel, yyue tent; that leedist forth Joseph as a scheep. Thou that sittist on cherubym; be schewid bifore Effraym,
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
Beniamyn, and Manasses. Stire thi power, and come thou; that thou make vs saaf.
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
God of vertues, turne thou vs; and schewe thi face, and we schulen be saaf.
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
Lord God of vertues; hou longe schalt thou be wrooth on the preier of thi seruaunt?
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
Hou longe schalt thou feede vs with the breed of teeris; and schalt yyue drynke to vs with teeris in mesure?
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
Thou hast set vs in to ayenseiyng to oure neiyboris; and oure enemyes han scornyde vs.
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
God of vertues, turne thou vs; and schewe thi face, and we schulen be saaf.
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
Thou translatidist a vyne fro Egipt; thou castidist out hethene men, and plauntidist it.
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
Thou were leeder of the weie in the siyt therof; and thou plauntidist the rootis therof, and it fillide the lond.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
The schadewe therof hilide hillis; and the braunchis therof filliden the cedris of God.
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
It streiyte forth hise siouns til to the see, and the generacioun ther of `til to the flood.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
Whi hast thou destried the wal therof; and alle men that goen forth bi the weie gaderiden awei the grapis therof?
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
A boor of the wode distriede it; and a singuler wielde beeste deuouride it.
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
God of vertues, be thou turned; biholde thou fro heuene, and se, and visite this vyne.
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
And make thou it perfit, which thi riythond plauntide; and biholde thou on the sone of man, which thou hast confermyd to thee.
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
Thingis brent with fier, and vndurmyned; schulen perische for the blamyng of thi cheer.
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Thin hond be maad on the man of thi riythond; and on the sone of man, whom thou hast confermed to thee.
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
And we departiden not fro thee; thou schalt quykene vs, and we schulen inwardli clepe thi name.
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Lord God of vertues, turne thou vs; and schewe thi face, and we schulen be saaf.

< Zaburi 80 >