< Zaburi 80 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
To the choirmaster to Shoshannim eduth of Asaph a psalm. O shepherd of Israel - give ear! O [you who] lead like flock Joseph O [you who] sit the cherubim shine forth!
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
Before Ephraim - and Benjamin and Manasseh stir up! might your and come! for salvation of us.
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
O God restore us and make shine face your so let us be delivered.
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
O Yahweh God of hosts until when? have you smoked at [the] prayer of people your.
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
You have fed them bread of tear[s] and you have made drink them tears a third of a measure.
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
You make us a contention to neighbors our and enemies our they mock themselves.
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
O God of hosts restore us and make shine face your so let us be delivered.
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
A vine from Egypt you uprooted you drove out nations and you planted it.
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
You made clear before it and it took root roots its and it filled [the] land.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
They were covered mountains shade its and branches its [the] cedars of God.
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
It stretched out branch[es] its to [the] sea and to [the] river young shoots its.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
Why? have you broken down walls its and they have plucked it all [those who] pass by of [the] road.
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
It eats away it wild boar from [the] forest and moving creature[s] of [the] field it grazes on it.
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
O God of hosts return please pay attention from heaven and see and attend to vine this.
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
And [the] root which it planted right [hand] your and on [the] son [whom] you made strong for yourself.
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
[it is] burned With fire [it is] cut down from [the] rebuke of face your they will perish.
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
May it be hand your on [the] man of right [hand] your on [the] son of humankind [whom] you have made strong for yourself.
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
And not we will turn back from you you will give life us and on name your we will call.
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
O Yahweh God of hosts restore us make shine face your so let us be delivered.