< Zaburi 80 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
“To the chief musician upon Shoshannim; an 'Eduth by Assaph; a psalm.” O Shepherd of Israel, give ear, thou that leadest Joseph like a flock; thou that dwellest between the cherubims, shine forth.
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
Before Ephraim and Benjamin and Menasseh awaken thy might, and come to our help.
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
O God, cause us to return, and let thy countenance shine, that we may be saved.
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
O Lord of hosts, how long shall thy anger smoke against the prayer of thy people?
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
Thou feedest them with the bread of tears, and givest them tears to drink in great measure.
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
Thou renderest us a contest unto our neighbors: and our enemies hold derision among themselves.
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
O God of hosts, cause us to return, and let thy countenance shine, that we may be saved.
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
A vine didst thou remove out of Egypt: thou drovest out nations, and plantedst it.
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
Thou didst clear out a place before it, and it struck its root deeply, and it filled the land.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
Mountains were covered with its shadow, and with its boughs the cedars of God.
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
It sent out its tendrils as far as the sea, and unto the river its suckers.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
Wherefore hast thou now broken down its fences, so that all who pass by the way pluck the fruit from it?
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
The boar out of the forest doth gnaw at it, and what moveth on the field feedeth on it.
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
O God of hosts, return; I pray thee, look down from heaven, and behold, and think of this vine;
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
And of the sprout which thy right hand hath planted, and of the branch that thou hast made strong for thyself.
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
It is burnt with fire, it is hewn down; because of the rebuke of thy countenance do they perish.
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Let thy hand be over the man of thy right hand, over the son of man whom thou hast made strong for thyself.
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
Then will we not swerve from thee: revive us again, and we will call on thy name.
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
O Lord God of hosts, cause us to return: let thy countenance shine, that we may be saved.