< Zaburi 80 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
For the Leader; upon Shoshannim. A testimony. A Psalm of Asaph. Give ear, O Shepherd of Israel, Thou that leadest Joseph like a flock; Thou that art enthroned upon the cherubim, shine forth.
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
Before Ephraim and Benjamin and Manasseh, stir up Thy might, and come to save us.
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
O God, restore us; and cause Thy face to shine, and we shall be saved.
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
O LORD God of hosts, how long wilt Thou be angry against the prayer of Thy people?
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
Thou hast fed them with the bread of tears, and given them tears to drink in large measure.
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
Thou makest us a strife unto our neighbours; and our enemies mock as they please.
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
O God of hosts, restore us; and cause Thy face to shine, and we shall be saved.
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
Thou didst pluck up a vine out of Egypt; Thou didst drive out the nations, and didst plant it.
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
Thou didst clear a place before it, and it took deep root, and filled the land.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
The mountains were covered with the shadow of it, and the mighty cedars with the boughs thereof.
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
She sent out her branches unto the sea, and her shoots unto the River.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
Why hast Thou broken down her fences, so that all they that pass by the way do pluck her?
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
The boar out of the wood doth ravage it, that which moveth in the field feedeth on it.
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
O God of hosts, return, we beseech Thee; look from heaven, and behold, and be mindful of this vine,
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
And of the stock which Thy right hand hath planted, and the branch that Thou madest strong for Thyself.
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
It is burned with fire, it is cut down; they perish at the rebuke of Thy countenance.
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Let Thy hand be upon the man of Thy right hand, upon the son of man whom Thou madest strong for Thyself.
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
So shall we not turn back from Thee; quicken Thou us, and we will call upon Thy name.
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
O LORD God of hosts, restore us; cause Thy face to shine, and we shall be saved.

< Zaburi 80 >