< Zaburi 80 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
For the music director. A psalm of Asaph. To the tune “Lilies of the Covenant.” Please hear us, Shepherd of Israel, you who lead the descendants of Joseph like a flock. You who sit on your throne above the cherubim, shine out
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
in the presence of Ephraim, Benjamin, and Manasseh. Gather together your power and come to save us!
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
God, please restore us! Let your face shine on us so we can be saved.
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
Lord God Almighty, how long will you be angry with the prayers of your people?
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
You fed them with the bread of tears, and gave them a full bowl of tears to drink.
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
You turn us into victims our neighbors fight over; our enemies mock us.
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
God Almighty, please restore us! Let your face shine on us so we can be saved!
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
You carried us out of Egypt like a vine. You drove out the heathen nations, and then you planted the vine.
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
You prepared the ground for the vine. It took root and filled the land.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
The mountains were covered by its shade; its branches covered the great cedars.
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
It sent its branches as far west as the Mediterranean Sea, and its shoots as far east as the Euphrates River.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
So why have you broken down the walls that protect it so that everyone who passes by can steal its fruit?
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
Wild pigs from the forest eat it, wild animals feed on it.
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
God Almighty, please return to us! Look down from heaven and see what's happening to us! Come and care for this vine
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
that you planted yourself, this son that you brought up yourself.
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
We, your vine, have been chopped down and burned. May those who did this die when you glare at them.
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Protect the man who stands beside you; strengthen the son you have chosen.
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
Then we will not turn away from you. Revive us so we can pray to you.
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Lord God Almighty, please restore us! Let your face shine on us so we can be saved.