< Zaburi 80 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
To the chief Musician. On Shoshannim-Eduth. Of Asaph. A Psalm. Give ear, O Shepherd of Israel, thou that leadest Joseph like a flock; thou that sittest [between] the cherubim, shine forth.
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
Before Ephraim and Benjamin and Manasseh, stir up thy strength, and come to our deliverance.
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
O God, restore us; and cause thy face to shine, and we shall be saved.
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
Jehovah, God of hosts, how long will thine anger smoke against the prayer of thy people?
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
Thou hast fed them with the bread of tears, and given them tears to drink in large measure:
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
Thou hast made us a strife unto our neighbours, and our enemies mock among themselves.
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
Restore us, O God of hosts; and cause thy face to shine, and we shall be saved.
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
Thou broughtest a vine out of Egypt; thou didst cast out the nations, and plant it:
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
Thou preparedst space before it, and it took deep root, and filled the land;
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
The mountains were covered with its shadow, and the branches thereof were [like] cedars of God;
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
It sent out its boughs unto the sea, and its shoots unto the river.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
Why hast thou broken down its fences, so that all who pass by the way do pluck it?
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
The boar out of the forest doth waste it, and the beast of the field doth feed off it.
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
O God of hosts, return, we beseech thee; look down from the heavens, and behold, and visit this vine;
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Even the stock which thy right hand hath planted, and the young plant thou madest strong for thyself.
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
It is burned with fire, it is cut down; they perish at the rebuke of thy countenance.
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Let thy hand be upon the man of thy right hand, upon the son of man whom thou hast made strong for thyself.
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
So will we not go back from thee. Revive us, and we will call upon thy name.
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Restore us, O Jehovah, God of hosts; cause thy face to shine, and we shall be saved.

< Zaburi 80 >