< Zaburi 80 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
For the choirmaster. To the tune of “The Lilies of the Covenant.” A Psalm of Asaph. Hear us, O Shepherd of Israel, who leads Joseph like a flock; You who sit enthroned between the cherubim, shine forth
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
before Ephraim, Benjamin, and Manasseh. Rally Your mighty power and come to save us.
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Restore us, O God, and cause Your face to shine upon us, that we may be saved.
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
O LORD God of Hosts, how long will Your anger smolder against the prayers of Your people?
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
You fed them with the bread of tears and made them drink the full measure of their tears.
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
You make us contend with our neighbors; our enemies mock us.
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
Restore us, O God of Hosts, and cause Your face to shine upon us, that we may be saved.
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
You uprooted a vine from Egypt; You drove out the nations and transplanted it.
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
You cleared the ground for it, and it took root and filled the land.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
The mountains were covered by its shade, and the mighty cedars with its branches.
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
It sent out its branches to the Sea, and its shoots toward the River.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
Why have You broken down its walls, so that all who pass by pick its fruit?
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
The boar from the forest ravages it, and the creatures of the field feed upon it.
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
Return, O God of Hosts, we pray! Look down from heaven and see! Attend to this vine—
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
the root Your right hand has planted, the son You have raised up for Yourself.
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
Your vine has been cut down and burned; they perish at the rebuke of Your countenance.
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Let Your hand be upon the man at Your right hand, on the son of man You have raised up for Yourself.
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
Then we will not turn away from You; revive us, and we will call on Your name.
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Restore us, O LORD God of Hosts; cause Your face to shine upon us, that we may be saved.

< Zaburi 80 >