< Zaburi 80 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
Zborovođi. Po napjevu “Ljiljan svjedočanstva”. Asafov. Psalam. Pastiru Izraelov, počuj, ti što vodiš Josipa k'o stado ovaca! Ti što sjediš nad kerubima, zablistaj
2 mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
pred Efrajimom, Benjaminom, Manašeom: probudi silu svoju, priteci nam u pomoć!
3 Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Bože, obnovi nas, razvedri lice svoje i spasi nas!
4 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
Jahve, Bože nad Vojskama, dokle ćeš plamtjeti, premda se moli narod tvoj?
5 Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
Dokle ćeš nas hraniti kruhom suza i obilno pojiti suzama?
6 Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
Dokle će se oko nas svađat' susjedi i rugat' nam se naši dušmani?
7 Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
Bože nad Vojskama, obnovi nas, razvedri lice svoje i spasi nas!
8 Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
Ti prenese čokot iz Egipta, pogane istjera, a njega zasadi.
9 Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
Ti mu tlo pripravi, i on pusti korijenje i napuni zemlju.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
Sjena mu prekri bregove, lozje mu k'o Božji cedrovi.
11 Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
Mladice svoje ispruži do mora i svoje ogranke do Rijeke.
12 Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
Zašto si mu srušio ogradu da ga beru svi što putem prolaze,
13 Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
da ga pustoši vepar iz šume, da ga pasu poljske zvijeri?
14 Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
Vrati se, Bože nad Vojskama, pogledaj s neba i vidi, obiđi ovaj vinograd:
15 mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
zakrili što zasadi desnica tvoja, sina kog za se odgoji!
16 Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
Oni koji ga spališe i posjekoše nek' izginu od prijetnje lica tvojega!
17 Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
Tvoja ruka nek' bude nad čovjekom desnice tvoje, nad sinom čovječjim kog za se odgoji!
18 Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
Nećemo se više odmetnuti od tebe; poživi nas, a mi ćemo zazivati ime tvoje.
19 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Jahve, Bože nad Vojskama, obnovi nas, razvedri lice svoje i spasi nas!