< Zaburi 8 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, Bwana wetu, tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote! Umeuweka utukufu wako juu ya mbingu.
למנצח על הגתית מזמור לדוד יהוה אדנינו מה אדיר שמך בכל הארץ אשר תנה הודך על השמים׃
2 Midomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao umeamuru sifa, kwa sababu ya watesi wako, kumnyamazisha adui na mlipiza kisasi.
מפי עוללים וינקים יסדת עז למען צורריך להשבית אויב ומתנקם׃
3 Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, mwezi na nyota, ulizoziratibisha,
כי אראה שמיך מעשי אצבעתיך ירח וכוכבים אשר כוננתה׃
4 mwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria, binadamu ni nani hata unamjali?
מה אנוש כי תזכרנו ובן אדם כי תפקדנו׃
5 Umemfanya chini kidogo kuliko viumbe wa mbinguni, ukamvika taji ya utukufu na heshima.
ותחסרהו מעט מאלהים וכבוד והדר תעטרהו׃
6 Umemfanya mtawala juu ya kazi za mikono yako; umeweka vitu vyote chini ya miguu yake.
תמשילהו במעשי ידיך כל שתה תחת רגליו׃
7 Mifugo na makundi yote pia, naam, na wanyama wa kondeni,
צנה ואלפים כלם וגם בהמות שדי׃
8 ndege wa angani na samaki wa baharini, naam, kila kiogeleacho katika njia za bahari.
צפור שמים ודגי הים עבר ארחות ימים׃
9 Ee Bwana, Bwana wetu, tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!
יהוה אדנינו מה אדיר שמך בכל הארץ׃

< Zaburi 8 >