< Zaburi 78 >

1 Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Masquil de Asaph. ESCUCHA, pueblo mío, mi ley: inclinad vuestro oído á las palabras de mi boca.
2 Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
Abriré mi boca en parábola; hablaré cosas reservadas de antiguo:
3 yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
Las cuales hemos oído y entendido; que nuestros padres nos [las] contaron.
4 Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
No las encubriremos á sus hijos, contando á la generación venidera las alabanzas de Jehová, y su fortaleza, y sus maravillas que hizo.
5 Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
El estableció testimonio en Jacob, y pusó ley en Israel; la cual mandó á nuestros padres que la notificasen á sus hijos;
6 ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
Para que [lo] sepa la generación venidera, y los hijos que nacerán; y [los que] se levantarán, [lo] cuenten á sus hijos;
7 Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
A fin de que pongan en Dios su confianza, y no se olviden de las obras de Dios, y guarden sus mandamientos:
8 Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
Y no sean como sus padres, generación contumaz y rebelde; generación que no apercibió su corazón, ni fué fiel para con Dios su espíritu.
9 Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
Los hijos de Ephraim armados, flecheros, volvieron [las espaldas] el día de la batalla.
10 Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
No guardaron el pacto de Dios, ni quisieron andar en su ley:
11 Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
Antes se olvidaron de sus obras, y de sus maravillas que les había mostrado.
12 Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
Delante de sus padres hizo maravillas en la tierra de Egipto, en el campo de Zoán.
13 Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
Rompió la mar, é hízolos pasar; é hizo estar las aguas como en un montón.
14 Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
Y llevólos de día con nube, y toda la noche con resplandor de fuego.
15 Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
Hendió las peñas en el desierto: y dióles á beber como de grandes abismos;
16 alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
Pues sacó de la peña corrientes, é hizo descender aguas como ríos.
17 Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
Empero aun tornaron á pecar contra él, enojando en la soledad al Altísimo.
18 Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
Pues tentaron á Dios en su corazón, pidiendo comida á su gusto.
19 Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
Y hablaron contra Dios, diciendo: ¿Podrá poner mesa en el desierto?
20 Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
He aquí ha herido la peña, y corrieron aguas, y arroyos salieron ondeando: ¿podrá también dar pan? ¿aparejará carne á su pueblo?
21 Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
Por tanto oyó Jehová, é indignóse: y encendióse el fuego contra Jacob, y el furor subió también contra Israel;
22 kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
Por cuanto no habían creído á Dios, ni habían confiado en su salud:
23 Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
A pesar de que mandó á las nubes de arriba, y abrió las puertas de los cielos,
24 akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
E hizo llover sobre ellos maná para comer, y dióles trigo de los cielos.
25 Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
Pan de nobles comió el hombre: envióles comida á hartura.
26 Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
Movió el solano en el cielo, y trajo con su fortaleza el austro.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
E hizo llover sobre ellos carne como polvo, y aves de alas como arena de la mar.
28 Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
E hízolas caer en medio de su campo, alrededor de sus tiendas.
29 Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
Y comieron, y hartáronse mucho: cumplióles pues su deseo.
30 Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
No habían quitado de sí su deseo, aun estaba su vianda en su boca,
31 hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
Cuando vino sobre ellos el furor de Dios, y mató los más robustos de ellos, y derribó los escogidos de Israel.
32 Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
Con todo esto pecaron aún, y no dieron crédito á sus maravillas.
33 Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
Consumió por tanto en nada sus días, y sus años en la tribulación.
34 Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
Si los mataba, entonces buscaban á Dios; entonces se volvían solícitos en busca suya.
35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
Y acordábanse que Dios era su refugio, y el Dios Alto su redentor.
36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
Mas le lisonjeaban con su boca, y con su lengua le mentían:
37 mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
Pues sus corazones no eran rectos con él, ni estuvieron firmes en su pacto.
38 Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
Empero él misericordioso, perdonaba la maldad, y no [los] destruía: y abundó para apartar su ira, y no despertó todo su enojo.
39 Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
Y acordóse que eran carne; soplo que va y no vuelve.
40 Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
¡Cuántas veces lo ensañaron en el desierto, lo enojaron en la soledad!
41 Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Y volvían, y tentaban á Dios, y ponían límite al Santo de Israel.
42 Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
No se acordaron de su mano, del día que los redimió de angustia;
43 siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
Cuando puso en Egipto sus señales, y sus maravillas en el campo de Zoán;
44 Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
Y volvió sus ríos en sangre, y sus corrientes, porque no bebiesen.
45 Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
Envió entre ellos una mistura de moscas que los comían, y ranas que los destruyeron.
46 Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
Dió también al pulgón sus frutos, y sus trabajos á la langosta.
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
Sus viñas destruyó con granizo, y sus higuerales con piedra;
48 Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
Y entregó al pedrisco sus bestias, y al fuego sus ganados.
49 Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
Envió sobre ellos el furor de su saña, ira y enojo y angustia, con misión de malos ángeles.
50 Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
Dispuso el camino á su furor; no eximió la vida de ellos de la muerte, sino que entregó su vida á la mortandad.
51 Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
E hirió á todo primogénito en Egipto, las primicias de las fuerzas en las tiendas de Châm.
52 Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
Empero hizo salir á su pueblo como ovejas, y llevólos por el desierto, como un rebaño.
53 Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
Y guiólos con seguridad, que no tuvieron miedo; y la mar cubrió á sus enemigos.
54 Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
Metiólos después en los términos de su santuario, en este monte que ganó su mano derecha.
55 Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
Y echó las gentes de delante de ellos, y repartióles una herencia con cuerdas; é hizo habitar en sus moradas á las tribus de Israel.
56 Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
Mas tentaron y enojaron al Dios Altísimo, y no guardaron sus testimonios;
57 Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
Sino que se volvieron, y se rebelaron como sus padres: volviéronse como arco engañoso.
58 Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
Y enojáronlo con sus altos, y provocáronlo á celo con sus esculturas.
59 Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
Oyólo Dios, y enojóse, y en gran manera aborreció á Israel.
60 Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
Dejó por tanto el tabernáculo de Silo, la tienda [en que] habitó entre los hombres;
61 Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
Y dió en cautividad su fortaleza, y su gloria en mano del enemigo.
62 Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
Entregó también su pueblo á cuchillo, y airóse contra su heredad.
63 Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
El fuego devoró sus mancebos, y sus vírgenes no fueron loadas en cantos nupciales.
64 makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
Sus sacerdotes cayeron á cuchillo, y sus viudas no lamentaron.
65 Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
Entonces despertó el Señor á la manera del que ha dormido, como un valiente que grita excitado del vino:
66 Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
E hirió á sus enemigos en las partes posteriores: dióles perpetua afrenta.
67 Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
Y desechó el tabernáculo de José, y no escogió la tribu de Ephraim;
68 lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
Sino que escogió la tribu de Judá, el monte de Sión, al cual amó.
69 Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
Y edificó su santuario á manera de eminencia, como la tierra que cimentó para siempre.
70 Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
Y eligió á David su siervo, y tomólo de las majadas de las ovejas:
71 Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
De tras las paridas lo trajo, para que apacentase á Jacob su pueblo, y á Israel su heredad.
72 Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.
Y apacentólos con entereza de su corazón; y pastoreólos con la pericia de sus manos.

< Zaburi 78 >