< Zaburi 78 >

1 Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Intellectus Asaph. Attendite popule meus legem meam: inclinate aurem vestram in verba oris mei.
2 Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
Aperiam in parabolis os meum: loquar propositiones ab initio.
3 yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
Quanta audivimus et cognovimus ea: et patres nostri narraverunt nobis.
4 Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
Non sunt occultata a filiis eorum, in generatione altera. Narrantes laudes Domini, et virtutes eius, et mirabilia eius quæ fecit.
5 Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
Et suscitavit testimonium in Iacob: et legem posuit in Israel. Quanta mandavit patribus nostris nota facere ea filiis suis:
6 ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
ut cognoscat generatio altera. Filii qui nascentur, et exurgent, et narrabunt filiis suis,
7 Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
Ut ponant in Deo spem suam, et non obliviscantur operum Dei: et mandata eius exquirant.
8 Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
Ne fiant sicut patres eorum: generatio prava et exasperans. Generatio, quæ non direxit cor suum: et non est creditus cum Deo spiritus eius.
9 Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
Filii Ephrem intendentes et mittentes arcum: conversi sunt in die belli.
10 Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
Non custodierunt testamentum Dei, et in lege eius noluerunt ambulare.
11 Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
Et obliti sunt benefactorum eius, et mirabilium eius quæ ostendit eis.
12 Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
Coram patribus eorum fecit mirabilia in terra Ægypti, in campo Taneos.
13 Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
Interrupit mare, et perduxit eos: et statuit aquas quasi in utre.
14 Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
Et deduxit eos in nube diei: et tota nocte in illuminatione ignis.
15 Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
Interrupit petram in eremo: et adaquavit eos velut in abysso multa.
16 alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
Et eduxit aquam de petra: et deduxit tamquam flumina aquas.
17 Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
Et apposuerunt adhuc peccare ei: in iram excitaverunt Excelsum in inaquoso.
18 Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
Et tentaverunt Deum in cordibus suis: ut peterent escas animabus suis.
19 Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
Et male locuti sunt de Deo: dixerunt: Numquid poterit Deus parare mensam in deserto?
20 Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
Quoniam percussit petram, et fluxerunt aquæ, et torrentes inundaverunt. Numquid et panem poterit dare, aut parare mensam populo suo?
21 Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
Ideo audivit Dominus, et distulit: et ignis accensus est in Iacob, et ira ascendit in Israel:
22 kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
Quia non crediderunt in Deo, nec speraverunt in salutari eius:
23 Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
Et mandavit nubibus desuper, et ianuas cæli aperuit.
24 akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
Et pluit illis manna ad manducandum, et panem cæli dedit eis.
25 Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
Panem angelorum manducavit homo: cibaria misit eis in abundantia.
26 Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
Transtulit Austrum de cælo: et induxit in virtute sua Africum.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
Et pluit super eos sicut pulverem carnes, et sicut arenam maris volatilia pennata.
28 Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
Et ceciderunt in medio castrorum eorum: circa tabernacula eorum.
29 Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
Et manducaverunt et saturati sunt nimis, et desiderium eorum attulit eis:
30 Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
non sunt fraudati a desiderio suo. Adhuc escæ eorum erant in ore ipsorum,
31 hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
et ira Dei ascendit super eos. Et occidit pingues eorum, et electos Israel impedivit.
32 Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
In omnibus his peccaverunt adhuc: et non crediderunt in mirabilibus eius.
33 Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
Et defecerunt in vanitate dies eorum: et anni eorum cum festinatione.
34 Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
Cum occideret eos, quærebant eum: et revertebantur, et diluculo veniebant ad eum.
35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
Et rememorati sunt quia Deus adiutor est eorum: et Deus excelsus redemptor eorum est.
36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
Et dilexerunt eum in ore suo, et lingua sua mentiti sunt ei:
37 mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
Cor autem eorum non erat rectum cum eo: nec fideles habiti sunt in testamento eius.
38 Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
Ipse autem est misericors, et propitius fiet peccatis eorum: et non disperdet eos. Et abundavit ut averteret iram suam: et non accendit omnem iram suam:
39 Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
Et recordatus est quia caro sunt: spiritus vadens, et non rediens.
40 Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
Quoties exacerbaverunt eum in deserto, in iram concitaverunt eum in inaquoso?
41 Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Et conversi sunt, et tentaverunt Deum: et Sanctum Israel exacerbaverunt.
42 Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
Non sunt recordati manus eius, die qua redemit eos de manu tribulantis,
43 siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
Sicut posuit in Ægypto signa sua, et prodigia sua in campo Taneos.
44 Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
Et convertit in sanguinem flumina eorum, et imbres eorum, ne biberent.
45 Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
Misit in eos cœnomyiam, et comedit eos: et ranam, et disperdidit eos.
46 Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
Et dedit ærugini fructus eorum: et labores eorum locustæ.
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
Et occidit in grandine vineas eorum: et moros eorum in pruina.
48 Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
Et tradidit grandini iumenta eorum: et possessionem eorum igni.
49 Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
Misit in eos iram indignationis suæ: indignationem, et iram, et tribulationem: immissiones per angelos malos.
50 Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
Viam fecit semitæ iræ suæ, non pepercit a morte animabus eorum: et iumenta eorum in morte conclusit.
51 Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
Et percussit omne primogenitum in terra Ægypti: primitias omnis laboris eorum in tabernaculis Cham.
52 Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
Et abstulit sicut oves populum suum: et perduxit eos tamquam gregem in deserto.
53 Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
Et deduxit eos in spe, et non timuerunt: et inimicos eorum operuit mare.
54 Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
Et induxit eos in montem sanctificationis suæ, montem, quem acquisivit dextera eius. Et eiecit a facie eorum Gentes: et sorte divisit eis terram in funiculo distributionis.
55 Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
Et habitare fecit in tabernaculis eorum tribus Israel.
56 Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
Et tentaverunt, et exacerbaverunt Deum excelsum: et testimonia eius non custodierunt.
57 Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
Et averterunt se, et non servaverunt pactum: quemadmodum patres eorum, conversi sunt in arcum pravum.
58 Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
In iram concitaverunt eum in collibus suis: et in sculptilibus suis ad æmulationem eum provocaverunt.
59 Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
Audivit Deus, et sprevit: et ad nihilum redegit valde Israel.
60 Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
Et repulit tabernaculum Silo, tabernaculum suum, ubi habitavit in hominibus.
61 Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
Et tradidit in captivitatem virtutem eorum: et pulchritudinem eorum in manus inimici.
62 Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
Et conclusit in gladio populum suum: et hereditatem suam sprevit.
63 Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
Iuvenes eorum comedit ignis: et virgines eorum non sunt lamentatæ.
64 makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
Sacerdotes eorum in gladio ceciderunt: et viduæ eorum non plorabantur.
65 Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
Et excitatus est tamquam dormiens Dominus, tamquam potens crapulatus a vino.
66 Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
Et percussit inimicos suos in posteriora: opprobrium sempiternum dedit illis.
67 Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
Et repulit tabernaculum Ioseph: et tribum Ephraim non elegit:
68 lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
Sed elegit tribum Iuda, montem Sion quem dilexit.
69 Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
Et ædificavit sicut unicornium sanctificium suum in terra, quam fundavit in sæcula.
70 Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
Et elegit David servum suum, et sustulit eum de gregibus ovium: de post fœtantes accepit eum.
71 Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
Pascere Iacob servum suum, et Israel hereditatem suam:
72 Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.
Et pavit eos in innocentia cordis sui: et in intellectibus manuum suarum deduxit eos.

< Zaburi 78 >