< Zaburi 78 >

1 Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
アサフのマスキールの歌 わが民よ、わが教を聞き、わが口の言葉に耳を傾けよ。
2 Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
わたしは口を開いて、たとえを語り、いにしえからの、なぞを語ろう。
3 yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
これはわれらがさきに聞いて知ったこと、またわれらの先祖たちがわれらに語り伝えたことである。
4 Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
われらはこれを子孫に隠さず、主の光栄あるみわざと、その力と、主のなされたくすしきみわざとをきたるべき代に告げるであろう。
5 Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
主はあかしをヤコブのうちにたて、おきてをイスラエルのうちに定めて、その子孫に教うべきことをわれらの先祖たちに命じられた。
6 ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
これは次の代に生れる子孫がこれを知り、みずから起って、そのまた子孫にこれを伝え、
7 Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
彼らをして神に望みをおき、神のみわざを忘れず、その戒めを守らせるためである。
8 Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
またその先祖たちのようにかたくなで、そむく者のやからとなり、その心が定まりなく、その魂が神に忠実でないやからとならないためである。
9 Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
エフライムの人々は武装し、弓を携えたが、戦いの日に引き返した。
10 Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
彼らは神の契約を守らず、そのおきてにしたがって歩むことを拒み、
11 Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
神がなされた事と、彼らに示されたくすしきみわざとを忘れた。
12 Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
神はエジプトの地と、ゾアンの野でくすしきみわざを彼らの先祖たちの前に行われた。
13 Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
神は海を分けて彼らを通らせ、水を立たせて山のようにされた。
14 Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
昼は雲をもって彼らを導き、夜は、よもすがら火の光をもって彼らを導かれた。
15 Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
神は荒野で岩を裂き、淵から飲むように豊かに彼らに飲ませ、
16 alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
また岩から流れを引いて、川のように水を流れさせられた。
17 Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
ところが彼らはなお神にむかって罪をかさね、荒野でいと高き者にそむき、
18 Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
おのが欲のために食物を求めて、その心のうちに神を試みた。
19 Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
また彼らは神に逆らって言った、「神は荒野に宴を設けることができるだろうか。
20 Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
見よ、神が岩を打たれると、水はほとばしりいで、流れがあふれた。神はまたパンを与えることができるだろうか。民のために肉を備えることができるだろうか」と。
21 Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
それゆえ、主は聞いて憤られた。火はヤコブにむかって燃えあがり、怒りはイスラエルにむかって立ちのぼった。
22 kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
これは彼らが神を信ぜず、その救の力を信用しなかったからである。
23 Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
しかし神は上なる大空に命じて天の戸を開き、
24 akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
彼らの上にマナを降らせて食べさせ、天の穀物を彼らに与えられた。
25 Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
人は天使のパンを食べた。神は彼らに食物をおくって飽き足らせられた。
26 Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
神は天に東風を吹かせ、み力をもって南風を導かれた。
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
神は彼らの上に肉をちりのように降らせ、翼ある鳥を海の砂のように降らせて、
28 Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
その宿営のなか、そのすまいのまわりに落された。
29 Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
こうして彼らは食べて、飽き足ることができた。神が彼らにその望んだものを与えられたからである。
30 Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
ところが彼らがまだその欲を離れず、食物がなお口の中にあるうちに、
31 hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
神の怒りが彼らにむかって立ちのぼり、彼らのうちの最も強い者を殺し、イスラエルのうちのえり抜きの者を打ち倒された。
32 Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
すべてこれらの事があったにもかかわらず、彼らはなお罪を犯し、そのくすしきみわざを信じなかった。
33 Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
それゆえ神は彼らの日を息のように消えさせ、彼らの年を恐れをもって過ごさせられた。
34 Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
神が彼らを殺されたとき、彼らは神をたずね、悔いて神を熱心に求めた。
35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
こうして彼らは、神は彼らの岩、いと高き神は彼らのあがないぬしであることを思い出した。
36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
しかし彼らはその口をもって神にへつらい、その舌をもって神に偽りを言った。
37 mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
彼らの心は神にむかって堅実でなく、神の契約に真実でなかった。
38 Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
しかし神はあわれみに富まれるので、彼らの不義をゆるして滅ぼさず、しばしばその怒りをおさえて、その憤りをことごとくふり起されなかった。
39 Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
また神は、彼らがただ肉であって、過ぎ去れば再び帰りこぬ風であることを思い出された。
40 Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
幾たび彼らは野で神にそむき、荒野で神を悲しませたことであろうか。
41 Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
彼らはかさねがさね神を試み、イスラエルの聖者を怒らせた。
42 Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
彼らは神の力をも、神が彼らをあだからあがなわれた日をも思い出さなかった。
43 siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
神はエジプトでもろもろのしるしをおこない、ゾアンの野でもろもろの奇跡をおこない、
44 Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
彼らの川を血に変らせて、その流れを飲むことができないようにされた。
45 Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
神ははえの群れを彼らのうちに送って彼らを食わせ、かえるを送って彼らを滅ぼされた。
46 Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
また神は彼らの作物を青虫にわたし、彼らの勤労の実をいなごにわたされた。
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
神はひょうをもって彼らのぶどうの木を枯らし、霜をもって彼らのいちじく桑の木を枯らされた。
48 Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
神は彼らの家畜をひょうにわたし、彼らの群れを燃えるいなずまにわたされた。
49 Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
神は彼らの上に激しい怒りと、憤りと、恨みと、悩みと、滅ぼす天使の群れとを放たれた。
50 Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
神はその怒りのために道を設け、彼らの魂を死から免れさせず、そのいのちを疫病にわたされた。
51 Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
神はエジプトですべてのういごを撃ち、ハムの天幕で彼らの力の初めの子を撃たれた。
52 Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
こうして神はおのれの民を羊のように引き出し、彼らを荒野で羊の群れのように導き、
53 Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
彼らを安らかに導かれたので彼らは恐れることがなかった。しかし海は彼らの敵をのみつくした。
54 Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
神は彼らをその聖地に伴い、その右の手をもって獲たこの山に伴いこられた。
55 Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
神は彼らの前からもろもろの国民を追い出し、その地を分けて嗣業とし、イスラエルの諸族を彼らの天幕に住まわせられた。
56 Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
しかし彼らはいと高き神を試み、これにそむいて、そのもろもろのあかしを守らず、
57 Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
そむき去って、先祖たちのように真実を失い、狂った弓のようにねじれた。
58 Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
彼らは高き所を設けて神を怒らせ、刻んだ像をもって神のねたみを起した。
59 Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
神は聞いて大いに怒り、イスラエルを全くしりぞけられた。
60 Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
神は人々のなかに設けた幕屋なるシロのすまいを捨て、
61 Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
その力をとりことならせ、その栄光をあだの手にわたされた。
62 Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
神はその民をつるぎにわたし、その嗣業にむかって大いなる怒りをもらされた。
63 Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
火は彼らの若者たちを焼きつくし、彼らのおとめたちは婚姻の歌を失い、
64 makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
彼らの祭司たちはつるぎによって倒れ、彼らのやもめたちは嘆き悲しむことさえしなかった。
65 Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
そのとき主は眠った者のさめたように、勇士が酒によって叫ぶように目をさまして、
66 Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
そのあだを撃ち退け、とこしえの恥を彼らに負わせられた。
67 Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
神はヨセフの天幕をしりぞけ、エフライムの部族を選ばず、
68 lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
ユダの部族を選び、神の愛するシオンの山を選ばれた。
69 Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
神はその聖所を高い天のように建て、とこしえに基を定められた地のように建てられた。
70 Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
神はそのしもべダビデを選んで、羊のおりから取り、
71 Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
乳を与える雌羊の番をするところからつれて来て、その民ヤコブ、その嗣業イスラエルの牧者とされた。
72 Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.
こうして彼は直き心をもって彼らを牧し、巧みな手をもって彼らを導いた。

< Zaburi 78 >