< Zaburi 78 >

1 Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Eine Unterweisung; von Asaph. Höre, mein Volk, meine Lehre, neiget eure Ohren zu den Reden meines Mundes!
2 Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
Ich will meinen Mund zu einem Spruche öffnen, will Rätsel vortragen aus alter Zeit,
3 yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
was wir gehört und gelernt und was unsre Väter uns erzählt haben.
4 Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
Es wurde ihren Söhnen nicht vorenthalten, sondern sie haben dem spätern Geschlecht den Ruhm des HERRN erzählt, seine Macht und seine Wunder, die er getan,
5 Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
nämlich, daß er ein Zeugnis aufstellte in Jakob und ein Gesetz gab in Israel, von welchem er unsern Vätern befahl, es ihren Kindern kundzutun,
6 ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
damit das spätere Geschlecht es wisse, die Kinder, die noch sollten geboren werden, und damit auch sie, wenn sie aufgewachsen wären, es ihren Kindern erzählten;
7 Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
daß diese auf Gott ihr Vertrauen setzten und nicht vergäßen die Taten Gottes und seine Gebote befolgten
8 Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
und nicht würden wie ihre Väter, ein abtrünniges und widerspenstiges Geschlecht, ein Geschlecht, das kein festes Herz hatte, und dessen Geist nicht treu war gegen Gott.
9 Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
Die Kinder Ephraims, geübte Bogenschützen, wandten um am Tage der Schlacht.
10 Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
Sie bewahrten den Bund Gottes nicht und wollten nicht nach seinem Gesetze wandeln.
11 Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
Und sie vergaßen seine Taten und seine Wunder, die er ihnen erzeigt.
12 Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
Vor ihren Vätern hatte er Wunder getan im Lande Ägypten, im Gefilde Zoan.
13 Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
Er spaltete das Meer und führte sie hindurch und türmte die Wasser auf wie einen Damm,
14 Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
und leitete sie bei Tag mit einer Wolke und während der ganzen Nacht mit einem hellen Feuer.
15 Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
Er spaltete Felsen in der Wüste und tränkte sie wie mit großen Fluten,
16 alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
und ließ Bäche aus dem Felsen hervorspringen und Wasser herabfließen in Strömen.
17 Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
Dennoch fuhren sie fort, wider ihn zu sündigen und den Höchsten zu erzürnen in der Wüste.
18 Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
Und sie versuchten Gott in ihrem Herzen, indem sie Speise forderten nach ihrem Gelüste.
19 Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
Und sie redeten wider Gott und sprachen: «Kann Gott einen Tisch bereiten in der Wüste?
20 Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
Siehe, er hat den Felsen geschlagen, daß Wasser flossen und Bäche sich ergossen. Kann er aber auch Brot geben? Wird er seinem Volke Fleisch verschaffen?»
21 Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
Darum, als der HERR das hörte, ward er entrüstet, und Feuer entbrannte wider Jakob, ja, Zorn stieg auf über Israel,
22 kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
weil sie Gott nicht glaubten und nicht auf seine Hilfe vertrauten.
23 Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
Und er gebot den Wolken droben und öffnete die Türen des Himmels;
24 akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
und er ließ Manna auf sie regnen zum Essen und gab ihnen Himmelskorn.
25 Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
Der Mensch aß Engelsbrot; er sandte ihnen Speise genug.
26 Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
Er erregte den Ostwind am Himmel und führte durch seine Kraft den Südwind herbei,
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
ließ Fleisch auf sie regnen wie Staub und beschwingte Vögel wie Sand am Meer,
28 Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
und ließ sie fallen mitten in ihr Lager, rings um ihre Wohnung her.
29 Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
Da aßen sie und wurden allzu satt; was sie gewünscht hatten, gewährte er ihnen.
30 Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
Sie hatten sich ihres Gelüstes noch nicht entschlagen, und ihre Speise war noch in ihrem Munde,
31 hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
als der Zorn Gottes sich wider sie erhob und die Fetten unter ihnen erwürgte und die Jungmannschaft Israels darniederstürzte.
32 Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
Trotz alledem sündigten sie weiter und glaubten nicht an seine Wunder.
33 Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
Darum ließ er ihre Tage wie einen Hauch vergehen und ihre Jahre durch plötzlichen Untergang.
34 Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
Wenn er sie tötete, so suchten sie ihn und kehrten sich wieder zu Gott
35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
und dachten daran, daß Gott ihr Fels sei, und Gott, der Höchste, ihr Erlöser.
36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
Aber sie heuchelten ihm mit ihrem Munde und logen mit ihren Zungen;
37 mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
denn ihr Herz war nicht aufrichtig gegen ihn, und sie hielten nicht treu an seinem Bund.
38 Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
Er aber war barmherzig und vergab die Schuld und vertilgte sie nicht und hat oftmals seinen Zorn abgewandt und nicht allen seinen Grimm erweckt;
39 Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
denn er dachte daran, daß sie Fleisch seien, ein Wind, der hinfährt und nicht wiederkehrt.
40 Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
Wie oft empörten sie sich wider ihn in der Wüste und betrübten ihn in der Einöde!
41 Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Und sie versuchten Gott immer wieder und kränkten den Heiligen Israels.
42 Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
Sie sind seiner Hand nicht eingedenk gewesen, des Tages, da er sie vom Feinde erlöste;
43 siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
da er seine Zeichen tat in Ägypten und seine Wunder im Gefilde Zoan;
44 Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
als er ihre Ströme in Blut verwandelte und ihre Bäche, so daß man nicht trinken konnte;
45 Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
da er Ungeziefer unter sie sandte, das sie fraß, und Frösche, die sie verderbten;
46 Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
da er den Fressern ihre Früchte gab und den Heuschrecken ihre Erzeugnisse;
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
da er ihre Weinstöcke mit Hagel schlug und ihre Maulbeerbäume mit Schlossen
48 Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
und ihr Vieh dem Hagel preisgab und ihre Herden den Wetterstrahlen;
49 Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
da er gegen sie die Glut seines Zornes entsandte, Grimm und Ungnade und Drangsal, Scharen von Unglücksengeln;
50 Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
da er seinem Zorn den Lauf ließ, ihre Seele nicht vor dem Tod bewahrte, sondern ihr Leben der Pest preisgab;
51 Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
da er alle Erstgeburt in Ägypten schlug, die Erstlinge ihrer Kraft in den Hütten Hams.
52 Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
Und er ließ sein Volk ausziehen wie Schafe und leitete sie wie eine Herde in der Wüste
53 Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
und führte sie sicher, daß sie sich nicht fürchteten; ihre Feinde aber bedeckte das Meer.
54 Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
Und er brachte sie in die Grenzen seines Heiligtums; zu diesem Berg, den seine Rechte erworben.
55 Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
Und er vertrieb vor ihnen her die Heiden und teilte ihnen das Erbe aus mit der Meßschnur und ließ in ihren Zelten die Stämme Israels wohnen.
56 Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
Aber sie versuchten und erzürnten den höchsten Gott und hielten seine Zeugnisse nicht,
57 Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
sondern wichen zurück und fielen ab wie ihre Väter; sie gingen fehl wie ein trügerischer Bogen.
58 Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
Und sie reizten ihn zum Zorn durch ihre Höhen und zur Eifersucht durch ihre Götzen.
59 Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
Gott hörte es und entrüstete sich und verabscheute Israel sehr.
60 Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
Und er verließ seine Wohnung zu Silo, das Zelt, wo er unter den Menschen wohnte,
61 Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
und gab seine Macht in Gefangenschaft und seine Herrlichkeit in Feindeshand,
62 Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
und überlieferte sein Volk dem Schwert und war entrüstet über sein Erbe.
63 Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
Seine Jünglinge hat das Feuer verzehrt, und seine Jungfrauen mußten ohne Brautlied bleiben.
64 makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
Seine Priester sind durchs Schwert gefallen, und seine Witwen konnten nicht weinen.
65 Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
Da erwachte der Herr wie ein Schlafender, wie ein Starker, der sich Mut zugetrunken.
66 Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
Und er schlug seine Feinde zurück, ewige Schande fügte er ihnen zu.
67 Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
Und er verwarf das Zelt Josephs und erwählte nicht den Stamm Ephraim,
68 lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
sondern erwählte den Stamm Juda, den Berg Zion, welchen er liebt.
69 Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
Und er baute sein Heiligtum wie Himmelshöhen, gleich der Erde, die er auf ewig gegründet hat.
70 Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
Und er erwählte seinen Knecht David und nahm ihn von den Schafhürden weg.
71 Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
Da er den tragenden Schafen nachging, holte er ihn, daß er weiden sollte Jakob, sein Volk, und Israel, sein Erbe.
72 Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.
Und er weidete sie mit aller Treue seines Herzens und leitete sie mit geschickter Hand.

< Zaburi 78 >