< Zaburi 78 >

1 Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Ein Lehrgedicht von Asaph. Gib acht, mein Volk, auf meine Belehrung,
2 Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
Ich will auftun meinen Mund zur Rede in Sprüchen, will Rätsel verkünden von der Vorzeit her.
3 yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
Was wir gehört und erfahren und unsere Väter uns erzählt haben,
4 Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
das wollen wir ihren Kindern nicht verschweigen, sondern dem künftgen Geschlecht verkünden die Ruhmestaten des HERRN und seine Stärke und die Wunder, die er getan hat.
5 Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
Denn er hat ein Zeugnis aufgerichtet in Jakob und festgestellt in Israel ein Gesetz, von dem er unsern Vätern gebot, es ihren Kindern kundzutun,
6 ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
auf daß die Nachwelt Kenntnis davon erhielte: die Kinder, die geboren würden, sollten aufstehn und ihren Kindern davon erzählen,
7 Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
daß sie auf Gott ihr Vertrauen setzten und die Taten Gottes nicht vergäßen und seine Gebote befolgten,
8 Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
daß sie nicht wie ihre Väter würden, ein trotziges und widerspenstiges Geschlecht, ein Geschlecht mit wankelmütigem Herzen, dessen Geist sich nicht zuverlässig zu Gott hielt.
9 Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
Ephraims Söhne, bogengerüstete Schützen, haben den Rücken gewandt am Tage des Kampfes.
10 Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
Sie hielten den gottgestifteten Bund nicht und wollten nicht wandeln in seinem Gesetz;
11 Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
nein, sie vergaßen seine Taten und seine Wunder, die er sie hatte sehen lassen.
12 Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
Vor ihren Vätern hatte er Wunder getan im Lande Ägypten, im Gefilde von Zoan.
13 Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
Er spaltete das Meer und ließ sie hindurchziehn und türmte die Wasser auf wie einen Wall;
14 Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
er leitete sie bei Tag durch die Wolke und während der ganzen Nacht durch Feuerschein;
15 Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
er spaltete Felsen in der Wüste und tränkte sie reichlich wie mit Fluten;
16 alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
Bäche ließ er aus dem Felsen hervorgehn und Wasser gleich Strömen niederfließen.
17 Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
Dennoch fuhren sie fort, gegen ihn zu sündigen, und widerstrebten dem Höchsten in der Wüste;
18 Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
ja, sie versuchten Gott in ihren Herzen, indem sie Speise verlangten für ihr Gelüst,
19 Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
und redeten gegen Gott mit den Worten: »Kann Gott wohl einen Tisch in der Wüste uns decken?
20 Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
Wohl hat er den Felsen geschlagen, daß Wasser flossen heraus und Bäche sich ergossen; doch wird er auch vermögen Brot zu geben oder Fleisch seinem Volke zu schaffen?«
21 Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
Drum, als der HERR das hörte, ergrimmte er: Feuer entbrannte gegen Jakob, und Zorn stieg auf gegen Israel,
22 kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
weil sie an Gott nicht glaubten und auf seine Hilfe nicht vertrauten.
23 Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
Und doch gebot er den Wolken droben und tat die Türen des Himmels auf,
24 akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
ließ Manna auf sie regnen zum Essen und gab ihnen himmlisches Brotkorn:
25 Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
Engelspeise aßen sie allesamt, Reisekost sandte er ihnen zur Sättigung.
26 Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
Hinfahren ließ er den Ostwind am Himmel und führte durch seine Kraft den Südwind herbei;
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
Fleisch ließ er auf sie regnen wie Staub und beschwingte Vögel wie Meeressand;
28 Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
mitten in ihr Lager ließ er sie fallen, rings um ihre Wohnungen her.
29 Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
Da aßen sie und wurden reichlich satt, und was sie gewünscht, gewährte er ihnen.
30 Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
Noch hatten sie ihres Gelüsts sich nicht entschlagen, noch hatten sie ihre Speise in ihrem Munde,
31 hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
da stieg der Ingrimm Gottes gegen sie auf und erwürgte die kräftigen Männer unter ihnen und streckte Israels junge Mannschaft zu Boden.
32 Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
Trotz alledem sündigten sie weiter und glaubten nicht an seine Wunder.
33 Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
Drum ließ er ihre Tage vergehn wie einen Hauch und ihre Jahre in angstvoller Hast.
34 Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
Wenn er sie sterben ließ, dann fragten sie nach ihm und kehrten um und suchten Gott eifrig
35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
und dachten daran, daß Gott ihr Fels sei und Gott, der Höchste, ihr Erlöser.
36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
Doch sie heuchelten ihm mit ihrem Munde und belogen ihn mit ihrer Zunge;
37 mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
denn ihr Herz hing nicht fest an ihm, und sie hielten nicht treu an seinem Bunde.
38 Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
Doch er war barmherzig, vergab die Schuld und vertilgte sie nicht, nein, immer wieder hielt er seinen Zorn zurück und ließ nicht seinen ganzen Grimm erwachen;
39 Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
denn er dachte daran, daß Fleisch sie waren, ein Windhauch, der hinfährt und nicht wiederkehrt.
40 Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
Wie oft widerstrebten sie ihm in der Wüste, kränkten sie ihn in der Öde!
41 Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Und immer aufs neue versuchten sie Gott und betrübten den Heiligen Israels.
42 Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
Sie dachten nicht mehr an seine starke Hand, an den Tag, wo er sie vom Bedränger erlöste,
43 siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
als er seine Zeichen in Ägypten tat, seine Wunder im Gefilde von Zoan.
44 Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
Er verwandelte dort in Blut ihre Ströme, so daß man ihr fließendes Wasser nicht trinken konnte;
45 Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
er sandte unter sie Ungeziefer, das sie fraß, und Frösche, die ihnen Verderben brachten;
46 Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
er gab ihre Ernte den Freßgrillen preis und die Frucht ihrer Arbeit den Heuschrecken;
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
er zerschlug ihre Reben mit Hagel, ihre Maulbeerfeigenbäume mit Schloßen;
48 Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
er gab ihr Vieh dem Hagel preis und ihren Besitz den Blitzen;
49 Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
er sandte gegen sie seines Zornes Glut, Wut und Grimm und Drangsal: eine Schar von Unglücksengeln;
50 Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
er ließ seinem Ingrimm freien Lauf, entzog ihre Seele nicht dem Tode, überließ vielmehr ihr Leben der Pest;
51 Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
er ließ alle Erstgeburt in Ägypten sterben, der Manneskraft Erstlinge in den Zelten Hams.
52 Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
Dann ließ er sein Volk ausziehn wie Schafe und leitete sie in der Wüste wie eine Herde
53 Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
und führte sie sicher, so daß sie nicht bangten; ihre Feinde aber bedeckte das Meer.
54 Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
So brachte er sie nach seinem heiligen Gebiet, in das Bergland, das er mit seiner Rechten erworben,
55 Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
und vertrieb vor ihnen her die Völker, verloste ihr Gebiet als erblichen Besitz und ließ in ihren Zelten die Stämme Israels wohnen.
56 Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
Doch sie versuchten und reizten Gott, den Höchsten, und hielten sich nicht an seine Gebote,
57 Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
sondern fielen ab und handelten treulos, ihren Vätern gleich; sie versagten wie ein trüglicher Bogen
58 Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
und erbitterten ihn durch ihren Höhendienst und reizten ihn zum Eifer durch ihre Götzenbilder.
59 Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
Als Gott es vernahm, ergrimmte er und verwarf Israel ganz und gar:
60 Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
er gab seine Wohnung in Silo auf, das Zelt, das er aufgeschlagen unter den Menschen;
61 Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
er ließ seine Macht in Gefangenschaft fallen und seine Zier in die Hand des Feindes;
62 Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
er gab sein Volk dem Schwerte preis und war entrüstet über sein Erbteil;
63 Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
seine jungen Männer fraß das Feuer, und seine Jungfraun blieben ohne Brautlied;
64 makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
seine Priester fielen durchs Schwert, und seine Witwen konnten keine Totenklage halten.
65 Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
Da erwachte der Allherr wie ein Schlafender, wie ein vom Wein übermannter Kriegsheld;
66 Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
er schlug seine Feinde von hinten und gab sie ewiger Schande preis.
67 Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
Auch verwarf er das Zelt Josephs und erwählte nicht den Stamm Ephraim,
68 lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
sondern erwählte den Stamm Juda, den Berg Zion, den er liebgewonnen;
69 Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
und er baute den ragenden Bergen gleich sein Heiligtum, fest wie die Erde, die er auf ewig gegründet.
70 Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
Dann erwählte er David, seinen Knecht, den er wegnahm von den Hürden des Kleinviehs;
71 Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
von den Mutterschafen holte er ihn, daß er Jakob weide, sein Volk, und Israel, seinen Erbbesitz.
72 Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.
Der weidete sie mit redlichem Herzen und leitete sie mit kundiger Hand.

< Zaburi 78 >