< Zaburi 78 >

1 Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Eine Unterweisung Asaphs. Höre, mein Volk, mein Gesetz; neigt eure Ohren zu der Rede meines Mundes!
2 Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
Ich will meinen Mund auftun zu Sprüchen und alte Geschichten aussprechen,
3 yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
die wir gehört haben und wissen und unsre Väter uns erzählt haben,
4 Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
daß wir's nicht verhalten sollten ihren Kindern, die hernach kommen, und verkündigten den Ruhm des HERRN und seine Macht und seine Wunder, die er getan hat.
5 Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
Er richtete ein Zeugnis auf in Jakob und gab ein Gesetz in Israel, das er unsern Vätern gebot zu lehren ihre Kinder,
6 ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
auf daß es die Nachkommen lernten und die Kinder, die noch sollten geboren werden; wenn sie aufkämen, daß sie es auch ihren Kinder verkündigten,
7 Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
daß sie setzten auf Gott ihre Hoffnung und nicht vergäßen der Taten Gottes und seine Gebote hielten
8 Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
und nicht würden wie ihre Väter, eine abtrünnige und ungehorsame Art, welchen ihr Herz nicht fest war und ihr Geist nicht treulich hielt an Gott,
9 Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
wie die Kinder Ephraim, die geharnischt den Bogen führten, abfielen zur Zeit des Streits.
10 Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
Sie hielten den Bund Gottes nicht und wollten nicht in seinem Gesetz wandeln
11 Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
und vergaßen seiner Taten und seiner Wunder, die er ihnen erzeigt hatte.
12 Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
Vor ihren Vätern tat er Wunder in Ägyptenland, im Felde Zoan.
13 Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
Er zerteilte das Meer und ließ sie hindurchgehen und stellte das Wasser wie eine Mauer.
14 Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
Er leitete sie des Tages mit einer Wolke und des Nachts mit einem hellen Feuer.
15 Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
Er riß die Felsen in der Wüste und tränkte sie mit Wasser die Fülle
16 alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
und ließ Bäche aus den Felsen fließen, daß sie hinabflossen wie Wasserströme.
17 Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
Dennoch sündigten sie weiter gegen ihn und erzürnten den Höchsten in der Wüste
18 Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
und versuchten Gott in ihrem Herzen, daß sie Speise forderten für ihre Seelen,
19 Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
und redeten gegen Gott und sprachen: “Ja, Gott sollte wohl können einen Tisch bereiten in der Wüste?
20 Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
Siehe, er hat wohl den Felsen geschlagen, daß Wasser flossen und Bäche sich ergossen; aber wie kann er Brot geben und seinem Volke Fleisch verschaffen?”
21 Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
Da nun das der HERR hörte, entbrannte er, und Feuer ging an in Jakob, und Zorn kam über Israel,
22 kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
daß sie nicht glaubten an Gott und hofften nicht auf seine Hilfe.
23 Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
Und er gebot den Wolken droben und tat auf die Türen des Himmels
24 akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
und ließ das Man auf sie regnen, zu essen, und gab ihnen Himmelsbrot.
25 Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
Sie aßen Engelbrot; er sandte ihnen Speise die Fülle.
26 Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
Er ließ wehen den Ostwind unter dem Himmel und erregte durch seine Stärke den Südwind
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
und ließ Fleisch auf sie regnen wie Staub und Vögel wie Sand am Meer
28 Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
und ließ sie fallen unter ihr Lager allenthalben, da sie wohnten.
29 Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
Da aßen sie und wurden allzu satt; er ließ sie ihre Lust büßen.
30 Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
Da sie nun ihre Lust gebüßt hatten und noch davon aßen,
31 hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
da kam der Zorn Gottes über sie und erwürgte die Vornehmsten unter ihnen und schlug darnieder die Besten in Israel.
32 Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
Aber über das alles sündigten sie noch mehr und glaubten nicht an seine Wunder.
33 Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
Darum ließ er sie dahinsterben, daß sie nichts erlangten und mußten ihr Leben lang geplagt sein.
34 Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
Wenn er sie erwürgte, suchten sie ihn und kehrten sich zu Gott
35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
und gedachten, daß Gott ihr Hort ist und Gott der Höchste ihr Erlöser ist,
36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
und heuchelten mit ihrem Munde und logen ihm mit ihrer Zunge;
37 mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
aber ihr Herz war nicht fest an ihm, und hielten nicht treulich an seinem Bund.
38 Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
Er aber war barmherzig und vergab die Missetat und vertilgte sie nicht und wandte oft seinen Zorn ab und ließ nicht seinen ganzen Zorn gehen.
39 Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
Denn er gedachte, daß sie Fleisch sind, ein Wind, der dahinfährt und nicht wiederkommt.
40 Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
Wie oft erzürnten sie ihn in der Wüste und entrüsteten ihn in der Einöde!
41 Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Sie versuchten Gott immer wieder und meisterten den Heiligen in Israel.
42 Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
Sie gedachten nicht an seine Hand des Tages, da er sie erlöste von den Feinden;
43 siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
wie er denn seine Zeichen in Ägypten getan hatte und seine Wunder im Lande Zoan;
44 Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
da er ihr Wasser in Blut wandelte, daß sie ihre Bäche nicht trinken konnten;
45 Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
da er Ungeziefer unter sie schickte, daß sie fraß, und Frösche, die sie verderbten,
46 Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
und gab ihre Gewächse den Raupen und ihre Saat den Heuschrecken;
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
da er ihre Weinstöcke mit Hagel schlug und ihre Maulbeerbäume mit Schloßen;
48 Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
da er ihr Vieh schlug mit Hagel und ihre Herden mit Wetterstrahlen;
49 Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
da er böse Engel unter sie sandte in seinem grimmigen Zorn und ließ sie toben und wüten und Leid tun;
50 Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
da er seinen Zorn ließ fortgehen und ihre Seele vor dem Tode nicht verschonte und übergab ihr Leben der Pestilenz;
51 Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
da er alle Erstgeburt in Ägypten schlug, die Erstlinge ihrer Kraft in den Hütten Hams,
52 Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
und ließ sein Volk ausziehen wie die Schafe und führte sie wie eine Herde in der Wüste.
53 Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
Und leitete sie sicher, daß sie sich nicht fürchteten; aber ihre Feinde bedeckte das Meer.
54 Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
Und er brachte sie zu seiner heiligen Grenze, zu diesem Berge, den seine Rechte erworben hat,
55 Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
und vertrieb vor ihnen her die Völker und ließ ihnen das Erbe austeilen und ließ in jener Hütten die Stämme Israels wohnen.
56 Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
Aber sie versuchten und erzürnten Gott den Höchsten und hielten ihre Zeugnisse nicht
57 Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
und fielen zurück und verachteten alles wie ihre Väter und hielten nicht, gleichwie ein loser Bogen,
58 Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
und erzürnten ihn mit ihren Höhen und reizten ihn mit ihren Götzen.
59 Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
Und da das Gott hörte, entbrannte er und verwarf Israel ganz,
60 Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
daß er seine Wohnung zu Silo ließ fahren, die Hütte, da er unter Menschen wohnte,
61 Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
und gab seine Macht ins Gefängnis und seine Herrlichkeit in die Hand des Feindes
62 Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
und übergab sein Volk ins Schwert und entbrannte über sein Erbe.
63 Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
Ihre junge Mannschaft fraß das Feuer, und ihre Jungfrauen mußten ungefreit bleiben.
64 makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
Ihre Priester fielen durchs Schwert, und waren keine Witwen, die da weinen sollten.
65 Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
Und der Herr erwachte wie ein Schlafender, wie ein Starker jauchzt, der vom Wein kommt,
66 Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
und schlug seine Feinde zurück und hängte ihnen ewige Schande an.
67 Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
Und er verwarf die Hütte Josephs und erwählte nicht den Stamm Ephraim,
68 lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
sondern erwählte den Stamm Juda, den Berg Zion, welchen er liebte.
69 Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
Und baute sein Heiligtum hoch, wie die Erde, die ewiglich fest stehen soll.
70 Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
Und erwählte seinen Knecht David und nahm ihn von den Schafställen;
71 Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
von den säugenden Schafen holte er ihn, daß er sein Volk Jakob weiden sollte und sein Erbe Israel.
72 Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.
Und er weidete sie auch mit aller Treue und regierte mit allem Fleiß.

< Zaburi 78 >