< Zaburi 78 >
1 Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Hymne d'Asaph. Mon peuple, écoute mes instructions! Prête l'oreille aux paroles de ma bouche!
2 Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
J'ouvrirai ma bouche pour prononcer des sentences; Je dirai les mystères des temps anciens.
3 yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
Ce que nous avons entendu et appris à connaître. Ce que nos pères nous ont raconté,
4 Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
Nous ne le cacherons point à leurs descendants. Nous raconterons à la génération future les oeuvres glorieuses de l'Éternel, Et sa puissance, et les merveilles qu'il a accomplies.
5 Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
Il se fit de Jacob le dépositaire de ses révélations; Il établit en Israël une loi. Qu'il ordonna à nos pères d'enseigner à leurs enfants,
6 ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
Pour qu'elle fût connue de la génération suivante, Des enfants qui naîtraient. Et qui viendraient à leur tour la raconter à leurs enfants.
7 Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
Ils apprendraient ainsi à mettre en Dieu leur confiance, A ne pas oublier les oeuvres du Dieu fort, A garder ses commandements,
8 Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
Et à ne pas devenir, comme leurs pères. Une génération indocile et rebelle. Une génération au coeur inconstant. Et dont l'esprit fut infidèle à Dieu.
9 Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
Les fils d'Éphraïm, archers habiles à lancer la flèche. Ont tourné le dos le jour du combat.
10 Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
Ils n'ont point observé l'alliance de Dieu, Et ils ont refusé de suivre sa loi.
11 Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
Ils ont oublié ses oeuvres. Et les prodiges dont il les avait rendus témoins.
12 Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
En présence de leurs pères, il avait accompli des merveilles Dans le pays d'Egypte, dans les campagnes de Tsoan.
13 Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
Il entr'ouvrit la mer pour leur livrer passage; Il dressa les eaux, pareilles à une digue.
14 Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
Il conduisit son peuple, le jour, par la nuée, Et toute la nuit par l'éclat du feu.
15 Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
Il fendit des rochers dans le désert, Et il en fit couler des torrents pour le désaltérer.
16 alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
De la pierre, il fit jaillir des ruisseaux; Il en fit sortir des eaux, abondantes comme des fleuves.,
17 Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
Mais ils continuèrent à pécher contre lui, A se révolter dans le désert contre le Très-Haut.
18 Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
Ils tentèrent Dieu dans leur coeur. En demandant une nourriture conforme à leur désir.
19 Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
Ils parlèrent contre Dieu, Et ils dirent: «Dieu pourrait-il Dresser une table dans le désert?
20 Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
Voici qu'il a frappé le rocher, et les eaux ont coulé, Et des torrents se sont répandus. Mais pourra-t-il donner du pain. Procurer de la viande à son peuple?»
21 Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
L'Éternel entendit ces murmures, et il en fut indigné; Son brûlant courroux s'alluma contre Jacob; Sa colère s'éleva contre Israël,
22 kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
Parce qu'ils n'avaient pas cru en Dieu Et qu'ils ne s'étaient pas confiés en son secours.
23 Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
Alors il donna ses ordres aux nuées d'en haut, Et il ouvrit les portes des cieux.
24 akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
Il fit pleuvoir sur eux la manne pour les nourrir, Et il leur donna le froment des cieux.
25 Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
Tous mangèrent le pain des forts; Il leur envoya des vivres à satiété.
26 Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
Il fit souffler le vent d'Orient dans les cieux. Et il fit lever par sa puissance le vent du Midi.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
Il fit pleuvoir sur eux de la chair, comme de la poussière. Et des oiseaux, nombreux comme le sable de la mer.
28 Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
Il les fit tomber au milieu de leur camp, Et tout autour de leurs tentes.
29 Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
Ils mangèrent et se rassasièrent abondamment; Il leur accorda tout ce qu'ils avaient désiré.
30 Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
Ils avaient à peine assouvi leur convoitise, La nourriture était encore dans leur bouche,
31 hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
Que la colère de Dieu s'éleva contre eux: Il fit périr les hommes les plus robustes. Et il abattit l'élite d'Israël.
32 Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
Cependant ils péchèrent encore contre Dieu, Et ils ne se laissèrent pas convaincre Par ses oeuvres merveilleuses.
33 Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
Alors il fit disparaître leurs jours comme une ombre: Il emporta leurs années dans une ruine soudaine.
34 Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
Quand il les faisait mourir, ils le recherchaient; Ils revenaient et s'empressaient de se tourner vers Dieu.
35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
Ils se souvenaient que Dieu était leur rocher, Et le Dieu Très-Haut leur rédempteur.
36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
Mais leurs lèvres le trompaient, Et leur langue lui mentait.
37 mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
Leur coeur ne lui était pas fermement attaché, Et ils n'étaient pas fidèles à son alliance.
38 Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
Mais lui, plein de compassion, pardonnait aux pécheurs Et il ne les détruisait point. Il retint souvent sa colère Et il ne laissa pas se déchaîner son courroux.
39 Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
Il se souvint qu'ils n'étaient que chair, Un souffle qui passe et ne revient plus.
40 Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
Que de fois ils se révoltèrent contre lui dans le désert, Et l'irritèrent dans la solitude!
41 Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Ils recommencèrent à tenter Dieu, Et à offenser le Saint d'Israël.
42 Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
Ils ne se souvinrent plus de ce qu'avait accompli sa main, Le jour où il les délivra de l'oppresseur,
43 siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
Quand il fit éclater ses prodiges parmi les Égyptiens, Et ses miracles dans les campagnes de Tsoan.
44 Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
Il changea leurs fleuves en sang. Et ils ne purent plus boire à leurs ruisseaux.
45 Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
Il envoya contre eux des moustiques qui les dévoraient. Et des grenouilles qui infectaient le pays.
46 Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
Il abandonna leurs récoltes aux sauterelles. Et le fruit de leur travail à leurs essaims.
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
Il fit périr leurs vignes par la grêle, Et leurs sycomores par la gelée.
48 Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
Il livra leur bétail à la grêle, Et leurs troupeaux à la foudre.
49 Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
Il déchaîna contre eux l'ardeur de son courroux, La fureur, l'indignation, la colère. Toute une armée d'anges de malheur.
50 Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
Il donna libre cours à sa colère, Et, loin de les préserver de la mort, Il livra leur vie à la destruction.
51 Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
Il frappa tous les premiers-nés de l'Egypte, Ces prémices de la virilité dans les tentes de Gham,
52 Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
Puis il emmena son peuple comme un troupeau de brebis; Il le conduisit comme un troupeau à travers le désert.
53 Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
Il dirigea les pas des Israélites, Les préservant de tout danger et de toute crainte. Tandis que la mer engloutissait leurs ennemis.
54 Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
Il les fit parvenir jusqu'à sa frontière sainte, Jusqu'à la montagne que sa main droite a conquise.
55 Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
Il chassa des nations devant eux; Il leur en partagea le territoire par le sort, Et il fit habiter les tribus d'Israël sous les tentes de l'ennemi.
56 Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
Mais les Israélites tentèrent le Dieu Très-Haut; Ils se révoltèrent contre lui, Et ils n'observèrent pas ses commandements.
57 Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
Ils firent défection et furent infidèles comme leurs pères; Ils se détournèrent, pareils à un arc perfide.
58 Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
Ils l'irritèrent par le culte des hauts-lieux; Et ils excitèrent sa jalousie par leurs idoles.
59 Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
A cette vue, Dieu fut indigné; Il prit Israël en profonde aversion.
60 Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
Il abandonna le tabernacle de Silo, La tente dont il avait fait sa demeure parmi les hommes.
61 Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
Il laissa emmener en captivité le siège de sa puissance; Il livra sa gloire aux mains de l'ennemi.
62 Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
Il abandonna son peuple à l'épée, Et s'irrita contre son héritage.
63 Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
Le feu dévora ses jeunes gens. Et ses vierges furent privées de chants nuptiaux.
64 makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
Ses sacrificateurs tombèrent sous les coups de l'épée. Et ses veuves ne purent pas pleurer les morts.
65 Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
Alors le Seigneur se réveilla, Comme un homme qui vient de dormir. Comme un guerrier à qui le vin ferait pousser des cris de joie.
66 Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
Il refoula ses adversaires; Il leur infligea un opprobre éternel.
67 Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
Mais il prit en aversion la tente de Joseph, Et il répudia la tribu d'Éphraïm.
68 lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
Il choisit la tribu de Juda, La montagne de Sion qu'il chérit.
69 Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
Il y bâtit son sanctuaire, indestructible comme les cieux, Et comme la terre, dont il a posé les fondements pour l'éternité.
70 Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
Il choisit David, son serviteur; Il le prit dans les bergeries.
71 Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
Il alla le chercher auprès des brebis qui allaitent. Pour faire de lui le berger de Jacob, son peuple. Et d'Israël, son héritage.
72 Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.
Ainsi David fut pour eux un berger au coeur intègre. Et il les conduisit d'une main prudente.