< Zaburi 78 >

1 Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Psaume de méditation d'Asaph. O mon peuple, attachez-vous à ma loi; inclinez votre oreille vers les paroles de ma bouche.
2 Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
J'ouvrirai ma bouche en paraboles; je dirai les choses qui ont existé dès le commencement,
3 yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
Telles que vous les avez ouïes et connues, et que vos pères vous les ont racontées.
4 Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
Elles n'ont point été cachées à leurs enfants de la seconde génération, eux-mêmes leur ayant annoncé les louanges du Seigneur, et sa puissance et les merveilles qu'il a faites.
5 Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
Et il a suscité un témoignage en Jacob, et il a institué en Israël une loi qu'il a confiée à nos pères, pour qu'ils l'enseignassent à leurs enfants,
6 ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
Afin que chaque génération les transmit à la suivante; les fils l'apprendront à ceux qui naîtront d'eux; et ils en porteront témoignage, et ils en instruiront leurs enfants:
7 Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
Afin qu'ils mettent en Dieu leur espérance, et qu'ils n'oublient point ses œuvres, et qu'ils recherchent ses commandements,
8 Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
Et qu'ils ne soient point comme leurs pères, race perverse et provocatrice, qui n'a pas eu de droiture de cœur, et, en son esprit, n'a pas été fidèle à Dieu.
9 Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
Les fils d'Éphraïm tendant l'arc, lançant des flèches, le jour du combat ont tourné le dos.
10 Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
Ils n'ont point gardé l'alliance de Dieu, et ils ont refusé de marcher dans sa loi.
11 Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
Et ils ont oublié ses bienfaits, et les miracles qu'il leur a montrés,
12 Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
Et les prodiges qu'il a faits devant leurs pères, en la terre d'Egypte et dans la plaine de Tanis.
13 Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
Il a séparé la mer, et il les a fait passer; il a contenu les eaux, comme dans une outre.
14 Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
Et il les a guidés le jour dans une nuée, et la nuit dans un luminaire de feu.
15 Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
Il a fendu le rocher dans le désert, et il les a abreuvés comme avec l'eau d'un grand abîme.
16 alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
Et de la pierre il a tiré et conduit l'eau comme un fleuve.
17 Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
Et ils ont continué de pécher contre lui; ils ont provoqué le Très-Haut dans le désert;
18 Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
Et ils ont tenté Dieu en leurs cœurs, en lui demandant des aliments pour leurs âmes.
19 Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
Et ils ont parlé contre Dieu, et ils ont dit: Est-ce que Dieu pourra nous préparer une table dans le désert?
20 Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
Il a frappé le rocher: l'eau a jailli; un torrent a coulé avec abondance. Mais Dieu pourra-t-il nous donner aussi du pain, ou préparer dans le désert une table à son peuple?
21 Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
C'est pourquoi le Seigneur, les ayant entendus, différa, et un feu fut allumé contre Jacob, et sa colère monta contre Israël;
22 kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
Parce qu'ils n'avaient pas eu foi en Dieu, et qu'ils n'avaient point espéré en sa protection.
23 Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
Et d'en haut il donna ses ordres aux nues, et il ouvrit les portes du ciel.
24 akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
Et il fit pleuvoir sur eux la manne pour les nourrir, et il leur donna le pain du ciel.
25 Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
L'homme mangea le pain des anges; Dieu leur envoya des aliments en abondance.
26 Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
Il chassa le vent du midi, et par sa puissance il amena le vent de l'occident.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
Et il fit pleuvoir pour eux de la chair comme des nuées de poussière, et des oiseaux emplumés comme le sable des mers.
28 Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
Et ces oiseaux tombèrent au milieu de leur camp, autour de leurs tentes.
29 Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
Et ils mangèrent, et ils furent rassasiés; et il satisfit leur désir.
30 Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
Rien ne leur manqua de ce qu'ils désiraient, et ils en avaient encore la bouche pleine.
31 hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
Et la colère du Seigneur s'éleva contre eux, et il mit à mort leurs riches, et il saisit les élus d'Israël.
32 Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
Et malgré tout cela ils péchèrent encore, et ne crurent point à ses prodiges.
33 Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
Et leurs jours défaillirent en vanité, et leurs années se précipitèrent.
34 Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
Quand il eut répandu parmi eux la mort, ils cherchèrent le Seigneur, et ils se convertirent à lui, et ils vinrent dès le matin vers Dieu.
35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
Et ils se souvinrent que Dieu est leur champion, et que Dieu le Très-Haut est leur rédempteur.
36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
Et ils l'aimèrent de la bouche; mais leur langue lui mentait.
37 mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
Car leur cœur ne fut point droit envers lui, et ils ne furent point fidèles en son alliance.
38 Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
Et cependant il est miséricordieux, et il leur remettra leurs péchés; et il ne les détruira point. Il détournera souvent sa colère, et son courroux ne s'enflammera pas tout entier.
39 Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
Et il se souvint qu'ils étaient chair, un souffle qui passe et ne revient plus.
40 Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
Combien de fois l'ont-ils provoqué dans le désert, et l'ont-ils irrité dans la terre sans eau!
41 Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Et ils se convertissaient, et ils recommençaient à tenter Dieu, et ils aigrissaient encore le Saint d'Israël.
42 Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
Ils avaient oublié sa main, et le jour où elle les avait tirés des mains de l'oppresseur;
43 siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
Et comment il avait fait ses miracles en Egypte, et ses prodiges dans la plaine de Tanis;
44 Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
Et comment il avait changé en sang leurs fleuves et leurs pluies, afin qu'ils ne pussent boire;
45 Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
Et comment il avait envoyé des mouches de chien qui les dévoraient, et des grenouilles qui les détruisaient.
46 Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
Ils avaient oublié la nielle attachée à leurs fruits, et les sauterelles dont ils avaient souffert,
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
Et la grêle détruisant leurs vignes, et la gelée faisant périr leurs mûriers,
48 Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
Et les grêlons exterminant leur bétail, et le feu consumant leurs richesses,
49 Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
Et sa colère et son indignation tombant sur eux; colère, fureur, afflictions, envois d'anges exterminateurs;
50 Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
Et la voie ouverte à son courroux, et son dessein de ne point épargner leur vie, et d'enclore leurs troupeaux, dans la mort;
51 Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
Et le coup dont fut frappé tout premier-né en la terre d'Egypte, prémices de leurs peines sous leurs tentes de Cham;
52 Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
Et le soin qu'il prit d'enlever son peuple comme des brebis, et de les conduire dans le désert, comme un troupeau;
53 Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
Et les espérances qu'il leur donna, et les craintes dont il les délivra, et la mer qui couvrit leurs ennemis.
54 Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
Et il les mena sur la montagne qu'il s'était consacrée, cette montagne que sa droite avait acquise. Et il chassa les nations devant leur face, et il leur distribua, à grandes mesures, la terre de leur héritage.
55 Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
Et il établit les tribus d'Israël dans les demeures des vaincus.
56 Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
Mais elles tentèrent et provoquèrent Dieu le Très-Haut; elles ne gardèrent point ses témoignages.
57 Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
Et son peuple, se détournant de lui, s'endurcit comme ses pères; il devint comme un arc tortu.
58 Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
Et ils provoquèrent la colère de Dieu sur leurs hauts lieux; et ils le rendirent jaloux par leurs images sculptées.
59 Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
Dieu les entendit et les méprisa, et réduisit à néant Israël.
60 Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
Et il répudia le tabernacle de Silo, son tabernacle où il résidait parmi les hommes.
61 Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
Et il livra à la captivité leur force, aux ennemis leur beauté.
62 Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
Et il exposa son peuple au glaive, et il dédaigna son propre héritage.
63 Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
La flamme dévora leurs jeunes hommes, et leurs vierges ne furent point pleurées.
64 makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
Leurs prêtres tombèrent sous le glaive, et leurs veuves ne furent point pleurées.
65 Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
Et le Seigneur s'éveilla comme un homme endormi, ou comme un riche après l'ivresse.
66 Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
Et il frappa ses ennemis comme ils tournaient le dos, et il les couvrit d'un opprobre éternel.
67 Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
Et il répudia le tabernacle de Joseph, et il ne choisit point la tribu d'Éphraïm.
68 lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
Et il choisit la tribu de Juda, et la montagne de Sion, qu'il a aimée.
69 Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
Et il bâtit son sanctuaire, fort comme la corne des licornes, en la terre qu'il a fondée pour les siècles des siècles.
70 Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
Et il choisit David son serviteur, et il le tira de la garde des troupeaux; il le prit tandis qu'il surveillait les brebis mères,
71 Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
Pour qu'il fût le pasteur de Jacob, son serviteur, et d'Israël, son héritage.
72 Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.
Et David prit soin d'eux en l'innocence de son cœur, et il les mena dans la voie selon l'intelligence de ses mains.

< Zaburi 78 >