< Zaburi 78 >
1 Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Une contemplation d'Asaph. Écoutez mon enseignement, mon peuple. Prêtez l'oreille aux paroles de ma bouche.
2 Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
J'ouvrirai ma bouche en une parabole. Je vais prononcer les sombres paroles de l'ancien temps,
3 yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
que nous avons entendus et connus, et nos pères nous l'ont dit.
4 Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
Nous ne les cacherons pas à leurs enfants, raconter à la génération à venir les louanges de Yahvé, sa force, et les merveilles qu'il a faites.
5 Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
Car il a établi une alliance en Jacob, et a nommé un enseignant en Israël, qu'il a ordonné à nos pères, qu'ils doivent les faire connaître à leurs enfants;
6 ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
afin que la génération à venir sache, même les enfants qui doivent naître; qui doivent se lever et le dire à leurs enfants,
7 Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
afin qu'ils mettent leur espoir en Dieu, et ne pas oublier les actions de Dieu, mais gardez ses commandements,
8 Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
et ne seront pas comme leurs pères... une génération têtue et rebelle, une génération qui n'a pas rendu son cœur loyal, dont l'esprit n'était pas ferme avec Dieu.
9 Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
Les fils d'Ephraïm, armés et portant des arcs, a fait marche arrière au jour de la bataille.
10 Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
Ils n'ont pas respecté l'alliance de Dieu, et ont refusé de marcher dans sa loi.
11 Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
Ils ont oublié ses actions, les merveilles qu'il leur avait montrées.
12 Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
Il a fait des choses merveilleuses aux yeux de leurs pères, dans le pays d'Égypte, dans les champs de Zoan.
13 Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
Il fendit la mer, et les fit passer. Il a fait en sorte que les eaux se dressent comme un tas.
14 Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
Pendant le jour, il les conduisait aussi avec une nuée, et toute la nuit avec une lumière de feu.
15 Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
Il a fendu des rochers dans le désert, et leur donnait à boire en abondance comme dans les profondeurs.
16 alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
Il a aussi fait jaillir des ruisseaux du rocher, et a fait couler les eaux comme des rivières.
17 Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
Pourtant, ils ont continué à pécher contre lui, pour se rebeller contre le Très-Haut dans le désert.
18 Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
Ils ont tenté Dieu dans leur cœur en demandant de la nourriture selon leur désir.
19 Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
Oui, ils ont parlé contre Dieu. Ils ont dit: « Dieu peut-il préparer une table dans le désert?
20 Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
Voici, il a frappé le rocher, et les eaux ont jailli, et les ruisseaux ont débordé. Peut-il aussi donner du pain? Fournira-t-il de la viande à son peuple? »
21 Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
Yahvé entendit et se mit en colère. Un feu a été allumé contre Jacob, La colère est aussi montée contre Israël,
22 kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
parce qu'ils ne croyaient pas en Dieu, et n'avait pas confiance en son salut.
23 Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
Pourtant, il a commandé les cieux en haut, et a ouvert les portes du ciel.
24 akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
Il fit pleuvoir sur eux la manne pour qu'ils la mangent, et leur a donné de la nourriture venant du ciel.
25 Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
L'homme a mangé le pain des anges. Il leur a envoyé de la nourriture à satiété.
26 Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
Il fit souffler dans le ciel le vent d'est. Par son pouvoir, il a guidé le vent du sud.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
Il a aussi fait pleuvoir sur eux de la viande comme de la poussière, des oiseaux ailés comme le sable des mers.
28 Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
Il les fit tomber au milieu de leur camp, autour de leurs habitations.
29 Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
Ils mangèrent donc, et furent rassasiés. Il leur a donné leur propre désir.
30 Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
Ils ne se sont pas détournés de leurs envies. Leur nourriture était encore dans leur bouche,
31 hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
quand la colère de Dieu s'est élevée contre eux, a tué certains de leurs plus forts, et a frappé les jeunes hommes d'Israël.
32 Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
Malgré tout cela, ils ont péché, et ne croyaient pas en ses merveilles.
33 Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
C'est pourquoi il a consumé leurs jours dans la vanité, et leurs années de terreur.
34 Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
Quand il les a tués, ils ont demandé après lui. Ils sont revenus et ont cherché Dieu avec ardeur.
35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
Ils se sont souvenus que Dieu était leur rocher, le Dieu Très-Haut, leur rédempteur.
36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
Mais ils l'ont flatté de leur bouche, et lui ont menti avec leur langue.
37 mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
Car leur cœur n'était pas droit avec lui, ils n'ont pas été fidèles à son alliance.
38 Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
Mais lui, qui est miséricordieux, pardonna l'iniquité et ne les détruisit pas. Oui, plusieurs fois, il a détourné sa colère, et n'a pas déclenché toute sa colère.
39 Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
Il s'est souvenu qu'ils n'étaient que chair, un vent qui passe et ne revient pas.
40 Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
Combien de fois se sont-ils rebellés contre lui dans le désert, et l'ont affligé dans le désert!
41 Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Ils se retournèrent et tentèrent Dieu, et ont provoqué le Saint d'Israël.
42 Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
Ils ne se sont pas souvenus de sa main, ni le jour où il les a rachetés à l'adversaire;
43 siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
comment il a placé ses signes en Égypte, ses merveilles dans le champ de Zoan,
44 Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
il a changé leurs fleuves en sang, et leurs ruisseaux, de sorte qu'ils ne pouvaient pas boire.
45 Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
Il envoya parmi eux des nuées de mouches, qui les dévorèrent; et des grenouilles, qui les ont détruits.
46 Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
Il a aussi donné leur accroissement à la chenille, et leur travail à la sauterelle.
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
Il a détruit leurs vignes par la grêle, leurs figuiers sycomores avec le gel.
48 Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
Il a aussi livré leur bétail à la grêle, et leurs troupeaux à de chauds coups de foudre.
49 Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
Il a jeté sur eux l'ardeur de sa colère, la colère, l'indignation et le trouble, et une bande d'anges du mal.
50 Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
Il a tracé un chemin pour sa colère. Il n'a pas épargné leur âme de la mort, mais ont donné leur vie à la peste,
51 Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
et frappa tous les premiers-nés d'Égypte, le chef de leur force dans les tentes de Ham.
52 Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
Mais il a conduit son propre peuple comme des moutons, et les a guidés dans le désert comme un troupeau.
53 Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
Il les a conduits en toute sécurité, de sorte qu'ils n'ont pas eu peur, mais la mer a submergé leurs ennemis.
54 Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
Il les amena jusqu'à la frontière de son sanctuaire, à cette montagne, que sa main droite avait prise.
55 Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
Il a aussi chassé les nations devant eux, les a attribués en héritage par ligne, et a fait habiter les tribus d'Israël dans leurs tentes.
56 Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
Pourtant, ils ont tenté et se sont rebellés contre le Dieu Très-Haut, et n'a pas gardé ses témoignages,
57 Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
mais ils se sont détournés, et ont agi avec perfidie comme leurs pères. Ils étaient tordus comme un arc trompeur.
58 Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
Car ils l'ont irrité par leurs hauts lieux, et l'ont rendu jaloux avec leurs images gravées.
59 Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
Lorsque Dieu a entendu cela, il s'est mis en colère, et abhorrait fortement Israël,
60 Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
de sorte qu'il abandonna la tente de Silo, la tente qu'il a placée parmi les hommes,
61 Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
et a livré sa force en captivité, sa gloire dans la main de l'adversaire.
62 Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
Il a aussi livré son peuple à l'épée, et était en colère contre son héritage.
63 Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
Le feu a dévoré leurs jeunes hommes. Leurs vierges n'ont pas eu de chanson de mariage.
64 makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
Leurs prêtres sont tombés par l'épée, et leurs veuves ne pouvaient pas pleurer.
65 Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
Alors le Seigneur se réveilla comme quelqu'un qui sort du sommeil, comme un homme puissant qui crie à cause du vin.
66 Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
Il a frappé ses adversaires en arrière. Il les a soumis à un reproche perpétuel.
67 Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
De plus, il rejeta la tente de Joseph, et n'a pas choisi la tribu d'Ephraïm,
68 lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
Mais il choisit la tribu de Juda, Le mont Sion qu'il aimait.
69 Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
Il a construit son sanctuaire comme les hauteurs, comme la terre qu'il a établie pour toujours.
70 Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
Il a aussi choisi David, son serviteur, et l'ont pris dans les bergeries;
71 Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
de suivre les brebis qui ont leurs petits, il l'a amené à être le berger de Jacob, son peuple, et Israël, son héritage.
72 Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.
Il a doncété leur berger selon l'intégrité de son cœur, et les a guidés par l'habileté de ses mains.