< Zaburi 78 >

1 Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Maskil to/for Asaph to listen [emph?] people my instruction my to stretch ear your to/for word lip my
2 Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
to open in/on/with proverb lip my to bubble riddle from front: old
3 yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
which to hear: hear and to know them and father our to recount to/for us
4 Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
not to hide from son: child their to/for generation last to recount praise LORD and strength his and to wonder his which to make: do
5 Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
and to arise: establish testimony in/on/with Jacob and instruction to set: appoint in/on/with Israel which to command [obj] father our to/for to know them to/for son: child their
6 ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
because to know generation last son: child to beget to arise: rise and to recount to/for son: child their
7 Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
and to set: make in/on/with God loin their and not to forget deed God and commandment his to watch
8 Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
and not to be like/as father their generation to rebel and to rebel generation not to establish: establish heart his and not be faithful with God spirit his
9 Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
son: descendant/people Ephraim to handle to shoot bow to overturn in/on/with day battle
10 Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
not to keep: obey covenant God and in/on/with instruction his to refuse to/for to go: walk
11 Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
and to forget wantonness his and to wonder his which to see: see them
12 Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
before father their to make: do wonder in/on/with land: country/planet Egypt land: country Zoan
13 Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
to break up/open sea and to pass: bring them and to stand water like heap
14 Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
and to lead them in/on/with cloud by day and all [the] night in/on/with light fire
15 Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
to break up/open rock in/on/with wilderness and to water: drink like/as abyss many
16 alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
and to come out: issue to flow from crag and to go down like/as river water
17 Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
and to add: again still to/for to sin to/for him to/for to rebel Most High in/on/with dryness
18 Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
and to test God in/on/with heart their to/for to ask food to/for soul: appetite their
19 Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
and to speak: speak in/on/with God to say be able God to/for to arrange table in/on/with wilderness
20 Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
look! to smite rock and to flow: flowing water and torrent: river to overflow also food: bread be able to give: give if: surely no to establish: prepare flesh to/for people his
21 Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
to/for so to hear: hear LORD and be angry and fire to kindle in/on/with Jacob and also face: anger to ascend: rise in/on/with Israel
22 kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
for not be faithful in/on/with God and not to trust in/on/with salvation his
23 Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
and to command cloud from above and door heaven to open
24 akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
and to rain upon them manna to/for to eat and grain heaven to give: give to/for them
25 Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
food: bread mighty: angel to eat man: anyone provision to send: depart to/for them to/for satiety
26 Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
to set out east in/on/with heaven and to lead in/on/with strength his south
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
and to rain upon them like/as dust flesh and like/as sand sea bird wing
28 Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
and to fall: fall in/on/with entrails: among camp his around to/for tabernacle his
29 Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
and to eat and to satisfy much and desire their to come (in): bring to/for them
30 Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
not be a stranger from desire their still food their in/on/with lip their
31 hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
and face: anger God to ascend: rise in/on/with them and to kill in/on/with fatness their and youth Israel to bow
32 Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
in/on/with all this to sin still and not be faithful in/on/with to wonder his
33 Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
and to end: expend in/on/with vanity day their and year their in/on/with dismay
34 Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
if to kill them and to seek him and to return: repent and to seek God
35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
and to remember for God rock their and El (Most High) (LORD) Most High to redeem: redeem their
36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
and to entice him in/on/with lip their and in/on/with tongue their to lie to/for him
37 mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
and heart their not to establish: establish with him and not be faithful in/on/with covenant his
38 Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
and he/she/it compassionate to atone iniquity: crime and not to ruin and to multiply to/for to return: repent face: anger his and not to rouse all rage his
39 Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
and to remember for flesh they(masc.) spirit: breath to go: walk and not to return: return
40 Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
like/as what? to rebel him in/on/with wilderness to hurt him in/on/with wilderness
41 Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
and to return: again and to test God and holy Israel to wound
42 Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
not to remember [obj] hand: power his day which to ransom them from enemy
43 siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
which to set: put in/on/with Egypt sign: miraculous his and wonder his in/on/with land: country Zoan
44 Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
and to overturn to/for blood stream their and to flow their not to drink [emph?]
45 Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
to send: depart in/on/with them swarm and to eat them and frog and to ruin them
46 Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
and to give: give to/for locust crops their and toil their to/for locust
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
to kill in/on/with hail vine their and sycamore their in/on/with frost
48 Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
and to shut to/for hail cattle their and livestock their to/for flash
49 Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
to send: let go in/on/with them burning anger face: anger his fury and indignation and distress deputation messenger: angel bad: harmful
50 Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
to envy path to/for face: anger his not to withhold from death soul: myself their and living thing their to/for pestilence to shut
51 Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
and to smite all firstborn in/on/with Egypt first: beginning strength in/on/with tent Ham
52 Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
and to set out like/as flock people his and to lead them like/as flock in/on/with wilderness
53 Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
and to lead them to/for security and not to dread and [obj] enemy their to cover [the] sea
54 Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
and to come (in): bring them to(wards) border: boundary holiness his mountain: mount this to buy right his
55 Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
and to drive out: drive out from face: before their nation and to fall: allot them in/on/with cord inheritance and to dwell in/on/with tent their tribe Israel
56 Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
and to test and to rebel [obj] God Most High and testimony his not to keep: obey
57 Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
and to turn and to act treacherously like/as father their to overturn like/as bow deceit
58 Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
and to provoke him in/on/with high place their and in/on/with idol their be jealous him
59 Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
to hear: hear God and be angry and to reject much in/on/with Israel
60 Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
and to leave tabernacle Shiloh tent to dwell in/on/with man
61 Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
and to give: give to/for captivity strength his and beauty his in/on/with hand: power enemy
62 Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
and to shut to/for sword people his and in/on/with inheritance his be angry
63 Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
youth his to eat fire and virgin his not to boast: praise
64 makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
priest his in/on/with sword to fall: kill and widow his not to weep
65 Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
and to awake like/as sleeping Lord like/as mighty man to overcome from wine
66 Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
and to smite enemy his back reproach forever: enduring to give: put to/for them
67 Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
and to reject in/on/with tent Joseph and in/on/with tribe Ephraim not to choose
68 lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
and to choose [obj] tribe Judah [obj] mountain: mount Zion which to love: lover
69 Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
and to build like to exalt sanctuary his like/as land: country/planet to found her to/for forever: enduring
70 Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
and to choose in/on/with David servant/slave his and to take: take him from fold flock
71 Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
from after to nurse to come (in): bring him to/for to pasture in/on/with Jacob people his and in/on/with Israel inheritance his
72 Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.
and to pasture them like/as integrity heart his and in/on/with understanding palm his to lead them

< Zaburi 78 >