< Zaburi 78 >
1 Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Poučna pjesma. Asafova. Poslušaj, narode moj, moju nauku, prikloni uho riječima usta mojih!
2 Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
Otvorit ću svoja usta na pouku, iznijet ću tajne iz vremena davnih.
3 yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
Ono što čusmo i saznasmo, što nam kazivahu oci,
4 Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
nećemo kriti djeci njihovoj, predat ćemo budućem koljenu: slavu Jahvinu i silu njegovu i djela čudesna što ih učini.
5 Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
Svjedočanstvo podiže on u Jakovu, Zakon postavi u Izraelu, da ono što naredi ocima našim oni djeci svojoj objave,
6 ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
da sazna budući naraštaj, i sinovi koji će se roditi da djeci svojoj kazuju
7 Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
da u Boga ufanje svoje stave i ne zaborave djela Božjih, već da vrše zapovijedi njegove,
8 Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
kako ne bi bili, kao oci njihovi, naraštaj buntovan, prkosan - naraštaj srcem nestalan i duhom Bogu nevjeran.
9 Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
Sinovi Efrajimovi, ratnici s lukom, u dan bitke okrenuše leđa.
10 Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
Saveza s Bogom ne održaše i ne htjedoše hoditi po Zakonu njegovu.
11 Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
Zaboraviše na djela njegova, na čudesa koja im pokaza.
12 Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
Pred njihovim ocima činio je znakove u Egiptu, u Soanskom polju.
13 Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
On more razdijeli i njih prevede, vode kao nasip uzdiže.
14 Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
Danju ih vodio oblakom, a svu noć ognjem blistavim.
15 Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
U pustinji hrid prolomi i napoji ih obilno kao iz bezdana.
16 alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
Iz stijene izbi potoke te izvede vode k'o velike rijeke.
17 Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
A oni jednako griješiše, prkosiše Višnjem u pustinji.
18 Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
Boga su kušali u srcima svojim ištuć' (jela) svojoj pohlepnosti.
19 Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
Prigovarali su Bogu i pitali: “Može li Gospod stol u pustinji prostrti?
20 Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
Eno, udari u hrid, i voda poteče i provreše potoci: a može li dati i kruha, i mesa pružiti svome narodu?”
21 Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
Kad to začu Jahve, gnjevom usplamtje: oganj se raspali protiv Jakova, srdžba se razjari protiv Izraela,
22 kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
jer ne vjerovaše Bogu niti se u njegovu pomoć uzdaše.
23 Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
Pa ozgo naredi oblaku i otvori brane nebeske,
24 akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
k'o kišu prosu na njih mÓanu da jedu i nahrani ih kruhom nebeskim.
25 Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
Čovjek blagovaše kruh Jakih; on im dade hrane do sitosti.
26 Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
Probudi na nebu vjetar istočni i svojom silom južnjak dovede.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
Prosu na njih mesa k'o prašine i ptice krilatice k'o pijeska morskoga.
28 Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
Padoše usred njihova tabora i oko šatora njihovih.
29 Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
Jeli su i nasitili se, želju njihovu on im ispuni.
30 Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
Još nisu svoju utažili pohlepu i jelo im još bješe u ustima,
31 hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
kad se srdžba Božja na njih raspali: pokosi smrću prvake njihove i mladiće pobi Izraelove.
32 Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
Uza sve to griješiše dalje i ne vjerovaše u čudesna djela njegova.
33 Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
I skonča im dane jednim dahom i njihova ljeta naglim svršetkom.
34 Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
Kad ih ubijaše, tražiše ga i opet pitahu za Boga;
35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
spominjahu se da je Bog hridina njihova i Svevišnji njihov otkupitelj.
36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
Ali ga opet ustima svojim varahu i jezikom svojim lagahu njemu.
37 mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
Njihovo srce s njime ne bijaše, nit' bijahu vjerni Savezu njegovu.
38 Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
A on im milosrdno grijeh praštao i nije ih posmicao; često je gnjev svoj susprezao da ne plane svom jarošću.
39 Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
Spominjao se da su pÓut i dah koji odlazi i ne vraća se više.
40 Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
Koliko mu prkosiše u pustinji i žalostiše ga u samotnom kraju!
41 Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Sve nanovo iskušavahu Boga i vrijeđahu Sveca Izraelova
42 Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
ne spominjuć' se ruke njegove ni dana kad ih od dušmana izbavi,
43 siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
ni znakova njegovih u Egiptu, ni čudesnih djela u polju Soanskom.
44 Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
U krv im pretvori rijeke i potoke, da ne piju.
45 Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
Posla na njih obade da ih žderu i žabe da ih more.
46 Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
I predade skakavcu žetvu njihovu, i plod muke njihove žderaču.
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
Vinograde im tučom udari, a mrazom smokvike njihove.
48 Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
I predade grÓadu njihova goveda i munjama stada njihova.
49 Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
Obori na njih svu žestinu gnjeva svog, jarost, bijes i nevolju: posla na njih anđele nesreće.
50 Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
I put gnjevu svojem otvori: ne poštedje im život od smrti, životinje im izruči pošasti.
51 Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
Pobi u Egiptu sve prvorođeno, prvence u šatorju Hamovu.
52 Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
I povede narod svoj kao ovce i vođaše ih kao stado kroz pustinju.
53 Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
Pouzdano ih je vodio te se nisu bojali, a more je prekrilo dušmane njihove.
54 Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
U Svetu zemlju svoju on ih odvede, na bregove što mu ih osvoji desnica.
55 Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
Pred njima istjera pogane, konopom im podijeli baštinu, pod šatorjem njihovim naseli plemena izraelska.
56 Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
A oni iskušavali i gnjevili Boga Višnjega i nisu držali zapovijedi njegovih.
57 Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
Otpadoše, iznevjeriše se k'o oci njihovi, k'o luk nepouzdan oni zatajiše.
58 Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
Na gnjev ga nagnaše svojim uzvišicama, na ljubomor navedoše kumirima svojim.
59 Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
Bog vidje i gnjevom planu, odbaci posve Izraela.
60 Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
I napusti boravište svoje u Šilu, Šator u kojem prebivaše s ljudima.
61 Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
Preda u ropstvo snagu svoju i svoju diku u ruke dušmanske.
62 Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
Narod svoj prepusti maču, raspali se na svoju baštinu.
63 Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
Mladiće njihove oganj proguta, ne udaše se djevice njihove.
64 makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
Svećenici njihovi padoše od mača, ne zaplakaše Óudove njihove.
65 Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
Tad se k'o oda sna trgnu Gospodin, k'o ratnik vinom savladan.
66 Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
Udari otraga dušmane svoje, sramotu im vječitu zadade.
67 Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
On odbaci šator Josipov i Efrajimovo pleme ne odabra,
68 lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
već odabra pleme Judino i goru Sion koja mu omilje.
69 Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
Sagradi Svetište k'o nebo visoko, k'o zemlju utemelji ga dovijeka.
70 Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
Izabra Davida, slugu svojega, uze ga od torova ovčjih;
71 Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
odvede ga od ovaca dojilica da pase Jakova, narod njegov, Izraela, baštinu njegovu.
72 Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.
I pasao ih je srcem čestitim i brižljivim rukama vodio.