< Zaburi 77 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa Yeduthuni. Zaburi ya Asafu. Nilimlilia Mungu ili anisaidie, nilimlilia Mungu ili anisikie.
亞薩的詩,照耶杜頓的作法,交與伶長。 我要向上帝發聲呼求; 我向上帝發聲,他必留心聽我。
2 Nilipokuwa katika taabu, nilimtafuta Bwana, usiku nilinyoosha mikono bila kuchoka na nafsi yangu ilikataa kufarijika.
我在患難之日尋求主; 我在夜間不住地舉手禱告; 我的心不肯受安慰。
3 Ee Mungu, nilikukumbuka wewe, nikalia kwa huzuni; nikatafakari, roho yangu ikadhoofika.
我想念上帝,就煩燥不安; 我沉吟悲傷,心便發昏。 (細拉)
4 Ulizuia macho yangu kufumba; nilikuwa nasumbuka, nikashindwa kusema.
你叫我不能閉眼; 我煩亂不安,甚至不能說話。
5 Nilitafakari juu ya siku zilizopita, miaka mingi iliyopita,
我追想古時之日, 上古之年。
6 nilikumbuka nilivyoimba nyimbo usiku. Moyo wangu ulitafakari na roho yangu ikauliza:
我想起我夜間的歌曲,捫心自問; 我心裏也仔細省察。
7 “Je, Bwana atakataa milele? Je, hatatenda mema tena?
難道主要永遠丟棄我, 不再施恩嗎?
8 Je, upendo wake usio na mwisho umetoweka milele? Je, ahadi yake imekoma nyakati zote?
難道他的慈愛永遠窮盡, 他的應許世世廢棄嗎?
9 Je, Mungu amesahau kuwa na huruma? Je, katika hasira amezuia huruma yake?”
難道上帝忘記開恩, 因發怒就止住他的慈悲嗎? (細拉)
10 Ndipo nikawaza, “Huu ndio udhaifu wangu: lakini nitakumbuka miaka ya mkono wa kuume wa Aliye Juu Sana.”
我便說:這是我的懦弱, 但我要追念至高者顯出右手之年代。
11 Nitayakumbuka matendo ya Bwana; naam, nitaikumbuka miujiza yako ya zamani.
我要提說耶和華所行的; 我要記念你古時的奇事。
12 Nitazitafakari kazi zako zote na kuyawaza matendo yako makuu.
我也要思想你的經營, 默念你的作為。
13 Ee Mungu, njia zako ni takatifu. Ni mungu yupi aliye mkuu kama Mungu wetu?
上帝啊,你的作為是潔淨的; 有何神大如上帝呢?
14 Wewe ndiwe Mungu utendaye miujiza, umeonyesha uwezo wako katikati ya mataifa.
你是行奇事的上帝; 你曾在列邦中彰顯你的能力。
15 Kwa mkono wako wenye nguvu umewakomboa watu wako, uzao wa Yakobo na Yosefu.
你曾用你的膀臂贖了你的民, 就是雅各和約瑟的子孫。 (細拉)
16 Maji yalikuona, Ee Mungu, maji yalikuona yakakimbia, vilindi vilitetemeka.
上帝啊,諸水見你, 一見就都驚惶; 深淵也都戰抖。
17 Mawingu yalimwaga maji, mbingu zikatoa ngurumo kwa radi, mishale yako ikametameta huku na huko.
雲中倒出水來; 天空發出響聲; 你的箭也飛行四方。
18 Ngurumo yako ilisikika katika upepo wa kisulisuli, umeme wako wa radi ukaangaza dunia, nchi ikatetemeka na kutikisika.
你的雷聲在旋風中; 電光照亮世界; 大地戰抖震動。
19 Njia yako ilipita baharini, mapito yako kwenye maji makuu, ingawa nyayo zako hazikuonekana.
你的道在海中; 你的路在大水中; 你的腳蹤無人知道。
20 Uliongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Mose na Aroni.
你曾藉摩西和亞倫的手引導你的百姓, 好像羊群一般。

< Zaburi 77 >