< Zaburi 76 >
1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
Para el músico jefe. Con instrumentos de cuerda. Un salmo de Asaf. Una canción. En Judá, Dios es conocido. Su nombre es grande en Israel.
2 Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
Su tabernáculo está también en Salem. Su morada en Sión.
3 Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
Allí rompió las flechas de fuego del arco, el escudo, la espada y las armas de guerra. (Selah)
4 Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
Glorioso eres, y excelente, más que montañas de caza.
5 Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
Los hombres valientes yacen saqueados, han dormido su último sueño. Ninguno de los hombres de guerra puede levantar las manos.
6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
Ante tu reprimenda, Dios de Jacob, tanto el carro como el caballo son arrojados a un sueño muerto.
7 Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
Tú, incluso tú, eres de temer. ¿Quién puede estar a tu vista cuando estás enfadado?
8 Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
Tú pronunciaste el juicio desde el cielo. La tierra temió y guardó silencio,
9 wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
cuando Dios se levantó para juzgar, para salvar a todos los afligidos de la tierra. (Selah)
10 Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
Ciertamente la ira del hombre te alaba. Los supervivientes de tu ira están contenidos.
11 Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
¡Haz votos a Yahvé, tu Dios, y cúmplelos! Que todos sus vecinos le traigan regalos a quien debe ser temido.
12 Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.
cortará el espíritu de los príncipes. Es temido por los reyes de la tierra.