< Zaburi 76 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
Para el director del coro: Un Salmo de Asaf. Un canto. Acompañamiento con instrumentos de cuerda. Dios tiene honra en Judá. Su nombre es grande en todo Israel.
2 Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
Él vive en Jerusalén y habita en Sión.
3 Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
Allí quebró las fechas encendidas, los escudos, la espada y las armas de guerra. (Selah)
4 Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
Tu luz es gloriosa y eres más majestuoso que las montañas eternas.
5 Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
Nuestros enemigos más valientes han sido saqueados. Ya duermen el sueño de la muerte. Incluso los más fuertes entre ellos no pudieron levantar una mano contra nosotros.
6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
A tu voz, Dios de Jacob, tanto el caballo como el jinete caen muertos.
7 Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
Todos te temen. ¿Quién podría mantenerse en pie ante tu ira?
8 Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
Anunciaste juicio desde el cielo. Todos en la tierra se espantaron y quedaron inmóviles
9 wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
cuando te levantaste para pronunciar juicio y salvar a los oprimidos de la tierra. (Selah)
10 Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
Incluso la ira humana contra ti te hace brillar, porque la usas como corona.
11 Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
Haz promesas a Dios y asegúrate de cumplirlas. Todos rinden tributo al Temible.
12 Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.
Porque él humilla a los líderes orgullosos. Y aterroriza a los reyes de la tierra.

< Zaburi 76 >