< Zaburi 76 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
Til sangmesteren på strengelek; en salme av Asaf; en sang. Gud er kjent i Juda, hans navn er stort i Israel.
2 Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
Og han reiste sin hytte i Salem og sin bolig på Sion.
3 Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
Der sønderbrøt han buens lyn, skjold og sverd og krig. (Sela)
4 Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
Strålende er du, herlig fremfor røverfjellene.
5 Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
Mennene med det sterke hjerte er blitt et rov; de sover sin søvn, og ingen av de veldige menn fant sine hender.
6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
Ved din trusel, Jakobs Gud, falt både vogn og hest i dyp søvn.
7 Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
Du - forferdelig er du, og hvem kan bli stående for ditt åsyn når du blir vred?
8 Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
Fra himmelen lot du høre dom; jorden fryktet og blev stille,
9 wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
da Gud reiste sig til dom for å frelse alle saktmodige på jorden. (Sela)
10 Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
For menneskets vrede blir dig til pris; med enda større vrede omgjorder du dig.
11 Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
Gjør løfter og gi Herren eders Gud det I har lovt! Alle de som er omkring ham, skal komme med gaver til den Forferdelige.
12 Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.
Han kuer fyrstenes stolte ånd, forferdelig for kongene på jorden.

< Zaburi 76 >