< Zaburi 76 >
1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
Per il Capo de’ Musici. Per strumenti a corda. Salmo di Asaf. Canto. Iddio è conosciuto in Giuda; il suo nome è grande in Israele.
2 Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
Il suo tabernacolo e in Salem, e la sua dimora in Sion.
3 Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
Quivi ha spezzato le saette dell’arco, lo scudo, la spada e gli arnesi di guerra. (Sela)
4 Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
Tremendo sei tu, o Potente, quando ritorni dalle montagne di preda.
5 Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
Gli animosi sono stati spogliati, han dormito il loro ultimo sonno, e tutti gli uomini prodi sono stati ridotti all’impotenza.
6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
Alla tua minaccia, o Dio di Giacobbe, carri e cavalli sono stati presi da torpore.
7 Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
Tu, tu sei tremendo; e chi può reggere davanti a te quando t’adiri?
8 Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
Dal cielo facesti udir la tua sentenza; la terra temette e tacque,
9 wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
quando Iddio si levò per far giudicio, per salvare tutti gl’infelici della terra. (Sela)
10 Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
Certo, il furore degli uomini ridonderà alla tua lode; ti cingerai degli ultimi avanzi dei loro furori.
11 Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
Fate voti all’Eterno, all’Iddio vostro, e adempiteli; tutti quelli che gli stanno attorno portin doni al Tremendo.
12 Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.
Egli recide lo spirito dei principi, egli è tremendo ai re della terra.