< Zaburi 76 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
למנצח בנגינת מזמור לאסף שיר נודע ביהודה אלהים בישראל גדול שמו׃
2 Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
ויהי בשלם סכו ומעונתו בציון׃
3 Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
שמה שבר רשפי קשת מגן וחרב ומלחמה סלה׃
4 Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
נאור אתה אדיר מהררי טרף׃
5 Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
אשתוללו אבירי לב נמו שנתם ולא מצאו כל אנשי חיל ידיהם׃
6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
מגערתך אלהי יעקב נרדם ורכב וסוס׃
7 Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
אתה נורא אתה ומי יעמד לפניך מאז אפך׃
8 Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
משמים השמעת דין ארץ יראה ושקטה׃
9 wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
בקום למשפט אלהים להושיע כל ענוי ארץ סלה׃
10 Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
כי חמת אדם תודך שארית חמת תחגר׃
11 Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
נדרו ושלמו ליהוה אלהיכם כל סביביו יובילו שי למורא׃
12 Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.
יבצר רוח נגידים נורא למלכי ארץ׃

< Zaburi 76 >