< Zaburi 76 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
למנצח בנגינת מזמור לאסף שיר ב נודע ביהודה אלהים בישראל גדול שמו
2 Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
ויהי בשלם סוכו ומעונתו בציון
3 Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
שמה שבר רשפי-קשת מגן וחרב ומלחמה סלה
4 Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
נאור אתה אדיר-- מהררי-טרף
5 Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
אשתוללו אבירי לב-- נמו שנתם ולא-מצאו כל-אנשי-חיל ידיהם
6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
מגערתך אלהי יעקב נרדם ורכב וסוס
7 Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
אתה נורא אתה--ומי-יעמד לפניך מאז אפך
8 Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
משמים השמעת דין ארץ יראה ושקטה
9 wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
בקום-למשפט אלהים-- להושיע כל-ענוי-ארץ סלה
10 Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
כי-חמת אדם תודך שארית חמת תחגר
11 Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
נדרו ושלמו ליהוה אלהיכם כל-סביביו--יבילו שי למורא
12 Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.
יבצר רוח נגידים נורא למלכי-ארץ

< Zaburi 76 >