< Zaburi 76 >
1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
Dieu est connu en Juda, son nom est grand en Israël.
2 Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
Son tabernacle est en Salem, et son domicile en Sion.
3 Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
C'est là qu'il a brisé les foudres de l'arc, le bouclier, l'épée et la bataille. (Sélah)
4 Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
Tu es brillant et magnifique, plus que les montagnes des ravisseurs.
5 Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
Ils ont été dépouillés, les hommes au cœur fort; ils ont dormi leur sommeil, et tous ces hommes vaillants n'ont plus trouvé leurs mains.
6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
A ta menace, ô Dieu de Jacob, chars et chevaux ont été frappés d'assoupissement.
7 Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
Tu es redoutable, toi! Et qui peut subsister devant toi, dès que paraît ta colère?
8 Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
Lorsque des cieux tu fais entendre ton jugement, la terre est effrayée et se tient en repos;
9 wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
Quand tu te lèves, ô Dieu, pour juger, pour délivrer tous les affligés de la terre. (Sélah)
10 Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
Certes, la fureur de l'homme tourne à ta louange, quand tu te revêts de tout ton courroux.
11 Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
Faites des vœux, acquittez-les à l'Éternel votre Dieu; que tous ceux qui l'environnent, apportent des dons au Redoutable.
12 Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.
Il abat l'orgueil des princes; il est redoutable aux rois de la terre.