< Zaburi 76 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
To the chief Musician on Neginoth, A Psalm [or] Song of Asaph. In Judah [is] God known: his name [is] great in Israel.
2 Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
In Salem also is his tabernacle, and his dwelling place in Zion.
3 Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
There he broke the arrows of the bow, the shield, and the sword, and the battle. (Selah)
4 Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
Thou [art] more glorious [and] excellent than the mountains of prey.
5 Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
The stout-hearted are spoiled, they have slept their sleep: and none of the men of might have found their hands.
6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
At thy rebuke, O God of Jacob, both the chariot and horse are cast into a dead sleep.
7 Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
Thou, [even] thou, [art] to be feared: and who may stand in thy sight when once thou art angry?
8 Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
Thou didst cause judgment to be heard from heaven; the earth feared, and was still,
9 wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
When God arose to judgment, to save all the meek of the earth. (Selah)
10 Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
Surely the wrath of man shall praise thee: the remainder of wrath wilt thou restrain.
11 Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
Vow, and pay to the LORD your God: let all that are about him bring presents to him that ought to be feared.
12 Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.
He shall cut off the spirit of princes: [he is] terrible to the kings of the earth.

< Zaburi 76 >