< Zaburi 76 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
“For the leader of the music. Upon stringed instruments. A Psalm of Asaph.” In Judah is God known; Great is his name in Israel.
2 Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
In Jerusalem is his tabernacle, And in Zion his dwelling-place.
3 Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
There brake he the lightning of the bow, The shield, the sword, and all the weapons of battle.
4 Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
More glorious and excellent art thou Than those mountains of robbers!
5 Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
Spoiled are the stout-hearted; They sank into their sleep; The hands of the mighty were powerless.
6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
Before thy rebuke, O God of Jacob! Fell chariot and horseman into a deep sleep!
7 Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
Thou, thou, O God! art terrible! Who can stand before thee in thine anger?
8 Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
Thou didst cause judgment to be heard from heaven; The earth trembled and was still,
9 wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
When God arose to judgment, To save all the oppressed of the earth!
10 Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
The wrath of man shall praise thee, When thou girdest on the whole of thy wrath!
11 Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
Make and perform vows to Jehovah, your God! Let all that dwell around him bring gifts to the terrible One,
12 Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.
Who casteth down the pride of princes, Who is terrible to the kings of the earth!

< Zaburi 76 >