< Zaburi 76 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
“To the chief musician on Neginoth, a psalm or song of Assaph.” In Judah hath God been made known: in Israel is his name great.
2 Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
And in Salem was his tabernacle made, and his dwelling-place in Zion.
3 Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
There broke he the shining arrows of the bow, shield, and sword, and battle. (Selah)
4 Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
Thou art more brilliant, more excellent than the mountains [full] of prey.
5 Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
Bereft of reason are the stouthearted, they slumber their sleep: and none of the men of might have found [the use of] their hands.
6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
From thy rebuke, O God of Jacob, lie in deep sleep both chariot and horse.
7 Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
Thou—thou art to be feared: and who may stand in thy sight when once thy anger [is kindled]?
8 Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
From heaven hast thou caused [thy] sentence to be heard: the earth feared, and became still,
9 wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
When God rose to judgment, to save all the lowly of the earth. (Selah)
10 Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
For the fury of man shall praise thee: the remainder of the fury wilt thou gird about thee.
11 Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
Make vows, and pay [them] unto the Lord your God, all ye that are round about him: let men bring presents unto him that exciteth fear.
12 Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.
He will cut down the spirit of the powerful: he is terrible to the kings of the earth.

< Zaburi 76 >