< Zaburi 76 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
For the Leader; with string-music. A Psalm of Asaph, a Song. In Judah is God known; His name is great in Israel.
2 Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
In Salem also is set His tabernacle, and His dwelling-place in Zion.
3 Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
There He broke the fiery shafts of the bow; the shield, and the sword, and the battle. (Selah)
4 Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
Glorious art Thou and excellent, coming down from the mountains of prey.
5 Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
The stout-hearted are bereft of sense, they sleep their sleep; and none of the men of might have found their hands.
6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
At Thy rebuke, O God of Jacob, they are cast into a dead sleep, the riders also and the horses.
7 Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
Thou, even Thou, art terrible; and who may stand in Thy sight when once Thou art angry?
8 Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
Thou didst cause sentence to be heard from heaven; the earth feared, and was still,
9 wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
When God arose to judgment, to save all the humble of the earth. (Selah)
10 Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
Surely the wrath of man shall praise Thee; the residue of wrath shalt Thou gird upon Thee.
11 Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
Vow, and pay unto the LORD your God; let all that are round about Him bring presents unto Him that is to be feared;
12 Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.
He minisheth the spirit of princes; He is terrible to the kings of the earth.

< Zaburi 76 >