< Zaburi 76 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
To the chief music-maker; put to Neginoth. A Psalm. Of Asaph. A Song. In Judah is the knowledge of God; his name is great in Israel,
2 Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
In Salem is his tent, his resting-place in Zion.
3 Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
There were the arrows of the bow broken, there he put an end to body-cover, sword, and fight. (Selah)
4 Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
You are shining and full of glory, more than the eternal mountains.
5 Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
Gone is the wealth of the strong, their last sleep has overcome them; the men of war have become feeble.
6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
At the voice of your wrath, O God of Jacob, deep sleep has overcome carriage and horse.
7 Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
You, you are to be feared; who may keep his place before you in the time of your wrath?
8 Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
From heaven you gave your decision; the earth, in its fear, gave no sound,
9 wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
When God took his place as judge, for the salvation of the poor on the earth. (Selah)
10 Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
The ... will give you praise; the rest of ...
11 Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
Give to the Lord your God what is his by right; let all who are round him give offerings to him who is to be feared.
12 Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.
He puts an end to the wrath of rulers; he is feared by the kings of the earth.

< Zaburi 76 >