< Zaburi 76 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
For the choirmaster. With stringed instruments. A Psalm of Asaph. A song. God is known in Judah; His name is great in Israel.
2 Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
His tent is in Salem, His dwelling place in Zion.
3 Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
There He shattered the flaming arrows, the shield and sword and weapons of war.
4 Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
You are resplendent with light, more majestic than mountains filled with game.
5 Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
The valiant lie plundered; they sleep their last sleep. No men of might could lift a hand.
6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
At Your rebuke, O God of Jacob, both horse and rider lie stunned.
7 Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
You alone are to be feared. When You are angry, who can stand before You?
8 Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
From heaven You pronounced judgment, and the earth feared and was still
9 wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
when God rose up to judge, to save all the lowly of the earth.
10 Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
Even the wrath of man shall praise You; with the survivors of wrath You will clothe Yourself.
11 Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
Make and fulfill your vows to the LORD your God; let all the neighboring lands bring tribute to Him who is to be feared.
12 Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.
He breaks the spirits of princes; He is feared by the kings of the earth.

< Zaburi 76 >