< Zaburi 75 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
Alabarte hemos, o! Dios, alabar te hemos; que cercano está tu nombre: cuenten todos tus maravillas.
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
Cuando yo tuviere tiempo, yo juzgaré rectamente.
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
La tierra se arruinaba, y sus moradores: yo compuse sus columnas. (Selah)
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
Dije a los malvados: No os enloquezcáis: y a los impíos: No alcéis el cuerno.
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
No levantéis en alto vuestro cuerno; no habléis con cerviz gruesa.
6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
Porque ni de oriente, ni de occidente, ni del desierto viene el ensalzamiento.
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
Porque Dios, que es el juez; a este abate, y a aquel ensalza.
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
Que el cáliz está en la mano de Jehová, y lleno de vino bermejo de mistura, y él derrama de aquí: ciertamente sus heces chuparán, y beberán todos los impíos de la tierra.
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
Y yo anunciaré siempre: cantaré alabanzas al Dios de Jacob.
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
Y quebraré todos los cuernos de los pecadores: y los cuernos del justo serán ensalzados.

< Zaburi 75 >