< Zaburi 75 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
В конец, да не растлиши, псалом песни Асафу. Исповемыся Тебе, Боже, исповемыся Тебе и призовем имя Твое: повем вся чудеса Твоя.
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
Егда прииму время, Аз правоты возсужду.
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
Растаяся земля и вси живущии на ней, Аз утвердих столпы ея.
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
Рех беззаконнующым, не беззаконнуйте: и согрешающым, не возносите рога.
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
Не воздвизайте на высоту рога вашего и не глаголите на Бога неправду:
6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
яко ниже от исход, ниже и запад, ниже от пустых гор.
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
Яко Бог судия есть: сего смиряет, и сего возносит.
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
Яко чаша в руце Господни, вина нерастворена исполнь растворения, и уклони от сея в сию: обаче дрождие его не истощися, испиют вси грешнии земли.
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
Аз же возрадуюся в век, воспою Богу Иаковлю:
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
и вся роги грешных сломлю, и вознесется рог праведнаго.

< Zaburi 75 >