< Zaburi 75 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
聖歌隊の指揮者によって、「滅ぼすな」というしらべにあわせてうたわせたアサフの歌、さんび 神よ、われらはあなたに感謝します。われらは感謝します。われらはあなたのみ名を呼び、あなたのくすしきみわざを語ります。
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
定まった時が来れば、わたしは公平をもってさばく。
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
地とすべてこれに住むものがよろめくとき、わたしはその柱を堅くする。 (セラ)
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
わたしは、誇る者には「誇るな」と言い、悪しき者には「角をあげるな、
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
角を高くあげるな、高慢な態度をもって語るな」と言う。
6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
上げることは東からでなく、西からでなく、また荒野からでもない。
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
それはさばきを行われる神であって、神はこれを下げ、かれを上げられる。
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
主の手には杯があって、よく混ぜた酒があわだっている。主がこれを注ぎ出されると、地のすべての悪しき者はこれを一滴も残さずに飲みつくすであろう。
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
しかしわたしはとこしえに喜び、ヤコブの神をほめうたいます。
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
悪しき者の角はことごとく切り離されるが正しい者の角はあげられるであろう。

< Zaburi 75 >