< Zaburi 75 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
Per il Capo de’ musici. “Non distruggere”. Salmo di Asaf. Canto. Noi ti celebriamo, o Dio, ti celebriamo; quelli che invocano il tuo nome narrano le tue maraviglie.
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
Quando verrà il tempo che avrò fissato, io giudicherò dirittamente.
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
Si dissolva la terra con tutti i suoi abitanti, io ne rendo stabili le colonne. (Sela)
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
Io dico agli orgogliosi: Non vi gloriate! e agli empi: non alzate il corno!
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
Non levate il vostro corno in alto, non parlate col collo duro!
6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
Poiché non è dal levante né dal ponente, né dal mezzogiorno che vien l’elevazione;
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
ma Dio è quel che giudica; egli abbassa l’uno ed innalza l’altro.
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
L’Eterno ha in mano una coppa, ove spumeggia un vino pien di mistura. Egli ne mesce; certo, tutti gli empi della terra ne succeranno e berranno le fecce.
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
Ma io proclamerò del continuo queste cose, salmeggerò all’Iddio di Giacobbe;
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
spezzerò tutta la potenza degli empi, ma la potenza de’ giusti sarà accresciuta.

< Zaburi 75 >