< Zaburi 75 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
למנצח אל תשחת מזמור לאסף שיר הודינו לך אלהים הודינו וקרוב שמך ספרו נפלאותיך׃
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
כי אקח מועד אני מישרים אשפט׃
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
נמגים ארץ וכל ישביה אנכי תכנתי עמודיה סלה׃
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
אמרתי להוללים אל תהלו ולרשעים אל תרימו קרן׃
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
אל תרימו למרום קרנכם תדברו בצואר עתק׃
6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
כי לא ממוצא וממערב ולא ממדבר הרים׃
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
כי אלהים שפט זה ישפיל וזה ירים׃
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
כי כוס ביד יהוה ויין חמר מלא מסך ויגר מזה אך שמריה ימצו ישתו כל רשעי ארץ׃
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
ואני אגיד לעלם אזמרה לאלהי יעקב׃
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
וכל קרני רשעים אגדע תרוממנה קרנות צדיק׃

< Zaburi 75 >