< Zaburi 75 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
למנצח אל-תשחת מזמור לאסף שיר ב הודינו לך אלהים--הודינו וקרוב שמך ספרו נפלאותיך
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
כי אקח מועד אני מישרים אשפט
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
נמגים ארץ וכל-ישביה אנכי תכנתי עמודיה סלה
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
אמרתי להוללים אל-תהלו ולרשעים אל-תרימו קרן
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
אל-תרימו למרום קרנכם תדברו בצואר עתק
6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
כי לא ממוצא וממערב ולא ממדבר הרים
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
כי-אלהים שפט זה ישפיל וזה ירים
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
כי כוס ביד-יהוה ויין חמר מלא מסך-- ויגר מזה אך-שמריה ימצו ישתו כל רשעי-ארץ
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
ואני אגיד לעלם אזמרה לאלהי יעקב
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
וכל-קרני רשעים אגדע תרוממנה קרנות צדיק

< Zaburi 75 >