< Zaburi 75 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
Au maître de chant. " Ne détruis pas! " Psaume d'Asaph. Cantique. Nous te louons, ô Dieu, nous te louons; ton nom est proche: on raconte tes merveilles.
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
" Quand le temps sera venu, je jugerai avec justice.
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
La terre est ébranlée avec tous ceux qui l'habitent; moi, j'affermis ses colonnes. " — Séla.
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
Je dis aux orgueilleux: Ne vous enorgueillissez pas! et aux méchants: Ne levez pas la tête!
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
Ne levez pas si haut la tête, ne parlez pas avec tant d'arrogance!
6 Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
Car ce n'est ni de l'orient, ni de l'occident; ni du désert des montagnes!...
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
Non; c'est Dieu qui exerce le jugement: il abaisse l'un et il élève l'autre.
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
Car il y a dans la main de Yahweh une coupe, où bouillonne un vin plein d'aromates. Et il en verse: oui, ils en suceront la lie, ils boiront, tous les méchants de la terre.
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
Et moi, je publierai à jamais, je chanterai les louanges du Dieu de Jacob.
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
Et j'abattrai toutes les cornes des méchants; et les cornes du juste seront élevées.

< Zaburi 75 >